1985 - 2007
12. Agizo Kuu
Support Pages
Index To All Lessons School of Finances
World Christian News
Who
Are We? Site Index
Katika Biblia Yako Soma
Mdo 1:1-26 na Mdo 2:1-4
Mstari Wa Kukariri
‘…Huyu Yesu
aliyechukuliwa kutoka kwenu kwenda juu mbinguni, atakuja jinsi iyo hiyo
mlivyomwona akienda zake mbinguni.’ (Mdo 1:11).
Baadaye Zungumzieni Jambo Hili
Ni kwa njia gani tunaweza
kumfuata Yesu kwa kupitapita tukifanya mema, tukihubiri na kufundisha? Je,
unaweza kutaja njia ngapi? Orodhesha vitu utakavyofanya baada ya hapo.
Jambo La Kufanya Kabla
Hatujakutana Tena
Kusanyikeni na kuombeana
kila mtu na mwenzake ili mpate kubatizwa kwa Roho Mtakatifu (au kujazwa tena na
Roho Mtakatifu) kama ilivyotukia mara kwa mara kwa kanisa la kwanza katika
Kitabu cha Matendo ya Mitume. Paulo anasema katika Efe 5:18, ‘…bali mjazwe
Roho’. Hapa inamaanisha kwamba mwendelee kujazwa na Roho Mtakatifu.
Kazi Ya Kuandika Ya Stashahada
Andika ukurasa mmoja au
mbili za maelezo ukiainisha Yerusalemu yako, Yudea yako, Samaria yako, na
miisho ya nchi kwako ni wapi.
Tafakari Neno Kwa Neno
Mdo 1:8
Tumia Dakika Moja Kuubadilisha Ulimwengu
Ombea taifa la Iran
Idadi
ya watu: 65,000,000; Yapo makabila 65;
Waislamu ni 99%; Kanisa linakua katika mateso.
Hakikisha umewafundisha wengine somo hili.
Kila mara
omba na kujiandaa ukiongezea mistari mingine ya Biblia
na mifano yako mwenyewe
ili kufanya somo lieleweke vizuri zaidi.
Katika Kitabu cha Matendo ya Mitume mlango wa kwanza tunagundua maagizo sita yenye nguvu na ambayo yanatuwezesha kumtumikia Mungu, na kuwahudumia vema watu wa ulimwengu huu.
1. Tenda Mema
Matendo 1:1 yatuambia kwamba Yesu alianza kufanya mambo fulani na kufundisha. Kazi hiyo bado hajaimaliza kwa sababu leo hii, akiwa kichwa, anafanya kazi kupitia mwili wake, yaani kanisa. Sisi tu mikono yake, miguu yake, macho yake, na midimo yake.
Baadhi ya madhehebu wanapenda kuwa midomo tu, lakini katika Mdo 10:38 tunaona kwamba Yesu alipakwa mafuta kutenda mema. Yeye alituonesha upendo mkuu wa Mungu kwa wanadamu kwa yale aliyoyatenda; na kisha alituelezea Mungu alivyo kwa maneno ya kinywa chake.
2. Ujazwe Roho Mtakatifu
Kwanini? Kwa sababu tunaambiwa katika Mdo 1:2 kwamba Yesu mwenyewe alihudumu kwa kumtegemea Roho Mtakatifu.
Kwanini jambo hili kuwa muhimu
kiasi hicho?
Yesu alipokuja duniani
akiwa mtoto mchanga, aliacha uweza wake wa kimbingu mbinguni (Flp 2:7).
Alipotamka neno au kufanya miujiza alifanya hivyo kama mwanadamu aliyejua
kuhudumu kwa uweza wa Roho Mtakatifu. Yesu anasema kwamba leo watu wanaweza
kufanya kazi alizozifanya, naam na hata zilizo kubwa kuliko hizo, kwa uweza
uleule wa Roho Mtakatifu (Yn 14:12).
Je, umejazwa Roho Mtakatifu?
Yesu alijua umuhimu wa
tukio hili ndio maana katika Mdo 1:5 anawaahidi wafuasi wake ubatizo wa Roho
Mtakatifu; maana yake kuzamishwa ndani ya Roho Mtakatifu (Mt 3:11-17) (Mdo
2:39).
Roho Mtakatifu anakuwezesha
Katika Mdo 1:8 Yesu
alisema wafuasi wake wangepokea dunamis yaani nguvu atakapowajilia Roho
Mtakatifu. Kutoka neno dunamis tunapata maneno yenye nguvu kama dynamo
na dynamite. Mamlaka, hata ile iliyotoka kwa Mungu, haina nguvu bila
Roho Mtakatifu. Roho Mtakatifu dunamis ni ule uweza wa kuonesha ile
mamlaka tuliyonayo.Unaweza kukumbuka jinsi wafuasi wa Yesu walivyomkimbia usiku
ule alipokamatwa. Lakini angalia jinsi mambo yalivyobadilika baada ya kujazwa
Roho Mtakatifu; walipata ujasiri wa ajabu. Mtazame Petro kama mfano mzuri (Mdo
2:14-).
Ni nini madhumuni ya uweza huo?
Roho Mtakatifu huja kwa
sababu moja, kushuhudia kwa uweza kwamba Yesu yu hai.
3. Uwe Shahidi
Shahidi ni nani? Iwapo magari mawili yangegongana na kisha madereva wa magari hayo kupigana; polisi watakapofika kwenye tukio watauliza, ‘Ni nani aliyeona?’ Kwa maneno mengine, ‘Ni nani aliyeshuhudia mambo hayo yakitukia?’ Polisi wanataka ushahidi. Wajibu wa shahidi ni kusema kile alichokiona na/au kusikia. Hapaswi kutoa maoni au mawazo yake; wala hapaswi kutoa hukumu. Hahusiki na lo lote tena baada ya kutoa ushahidi wake, ingawa ushahidi huo unaweza kusababisha mtu akafungwa au akaachiliwa huru. Huko ndiko kuwa shahidi kazi ambayo sisi tumewajibishwa kuifanya.
Tumeona nini?
Tumemwona Yesu akitenda
kazi ndani yetu; akisamehe,
akiponya na kubariki, na kwahiyo tunayo mengi ya kusema. Roho Mtakatifu
anafanya kazi kupitia maneno yetu akishawishi watu kwamba yale tunayoyasema ni
kweli. Wakiamini na kumpokea Yesu wanawekwa huru, la hawakuamini watabakia katika
utumwa wa dhambi na Shetani. Je, twende wapi kueleza habari hizi? Kila mmoja
wetu ameshagawiwa sehemu yake katika shamba la Bwana ili atumike (2 Kor 10:13).
Yerusalemu
Watu wengi lazima
wasimulie habari njema hizi kwa watu wa Yerusalemu ambayo ni ule mji wa
nyumbani kwao ambako wanaelewana lugha na kufahamiana mazingira yao (Lk 8:39).
Yudea na Samaria
Wengine wataitwa kwenda Yudea na Samaria ambayo ni miji au mikoa ya
jirani ambako wanatofautiana kidogo kwa lugha na pengine wasikubalike mara moja
kwa ajili ya tofauti ndogo ndogo.
Hata miisho ya nchi
Baadhi wameitwa kwenda
nchi za mbali mahali ambako mazingira yake ni tofauti kabisa; watu wake, hali
ya hewa, lugha, utamaduni, na hata vyakula ni tofauti kabisa. Lakini wanapokuwa
katika nchi hizo za ugenini hawaachi kusema kwamba Yesu yu hai.
4. Tenda Kazi Haraka
Tunapaswa kutenda kazi kwa bidii hata Yesu atakaporudi tena; maana atarudi tena kama malaika walivyoahidi ( Mdo 1:11). Tunapaswa kuongeza bidii kwa sababu kurudi kwake kumekaribia; baadhi ya dalili za kurudi kwake zimeonekana. Sasa ni wakati wa kuomba na kisha kuwaleta kwa Yesu ndugu na marafiki. Atakaporudi hatakuja tena kama mtoto mchanga bali atakuja kama Bwana na Mfalme atakayetawala miaka elfu moja. Katika utawala wake hapa duniani Yesu ataweka mambo sawa kwa kweli yake na haki yake, na hatimaye katika kukamilisha historia ya mwanadamu, ataumba mbingu mpya na nchi mpya.
5. Mfanye Yesu Kuwa Bwana Na Mfalme
Jambo hili ni muhimu kwa sababu katika Mdo 1:3 tunaambiwa kwamba Yesu alitumia siku 40 akiwafundisha wafuasi wake habari za Ufalme wa Mungu.
Ufalme maana yake anayetawala ni Mfalme; kwahiyo mahali po pote ambapo Yesu ni Bwana, utawala wa haki ya Mungu upo. Na mahali Yesu anapofanywa Mfalme maisha ya watu yanabadilika, familia zinabadilika, vijiji na kanisa pia.
6. Ombeni Bila Kukoma
Jambo la kwanza walilolifanya waamini wa kwanza, mara ya kwanza walipokuwa bila Yesu ni kurejesha mawasiliano naye kwa njia ya maombi.
Katika Mdo 1:12-15 tunaambiwa kwamba wafuasi wanawake pamoja na ndugu zake Yesu waliungana kuwa kitu kimoja, wakiomba bila kukoma. Maria, mama wa Yesu alifanya maombezi, akiongea na Mwanaye katika maombi. Kutoka katika Lk 24:49 tunajua kwamba maombi yao yalikuwa, “Njoo Roho Mtakatifu, utuwezeshe”, na kweli katika Mdo 2 walipokea jibu la nguvu.
7. Teua Viongozi Wapya
Katika Mdo 1:15-26 tunaona jinsi wafuasi wa Yesu walivyomchagua Mtume mwingine badala ya Yuda Iskariote. Walimchagua mtu aliyejua kwamba Yesu yu hai. Haifai mahali pakakosa kiongozi; watu wanahitaji mtu wa kuwapa maelekezo ili waweze kuzitumia nguvu zao za kiroho na za kimwili kwa ajili ya Injili. Kwahiyo iwapo Mungu amekupa changamoto ya kusimama na kuwajibika katika kazi yake, sema , “Ndiyo Bwana” hata leo.
Kwa
Kumalizia Omba Kwa Ajili Ya Watu
Wa Ulimwengu Ambao Hawajafikiwa Na Injili Ya Yesu Kristo
Burkina Faso (2) |
||
Jina la Watu |
Lugha Yao |
Idadi Yao |
Toussian (Win, Tusia) |
Toussian, Northern |
19,500 |
Viewo (Vige, Vigu, Viemo) |
Vigue (Viemo) |
10,000 |
Yarsi (Wala, Dagaari Jula) |
Yari (Dagaari-Jula, Wala) |
15,000 |
1985 - 2007
With many thanks to Pastor Dastan
Mboera, Dar es Salaaam, Tanzania
and EAPTC Nairobi, Kenya
for this revision and translation from the original English.
mboeradsk @ yahoo.com
© Dr Les Norman The DCI Trust, UK
Permission is granted to provide
copies at cost price for study purposes
but not for sale or commercial
purposes. Freely you have received, so please freely give.
Support Pages
Index To All Lessons School of Finances
World Christian News
Who
Are We? Site Index
www.dci.org.uk