1985 - 2007
14. Umisheni Ni Nini?
Usiniambie ni starehe kukaa nyumbani!
Support Pages
Index To All Lessons
School of Finances
World Christian News
Who
Are We?
Site Index
Katika Biblia Yako Soma
2 Kor 5:11-6:10
Mstari Wa Kukariri
Maana , upendo wa Kristo
watubidisha; maana tumehukumu hivi, ya kwamba mmoja alikufa kwa ajili ya
wote,basi walikufa wote; tena alikufa kwa ajili ya wote, ili walio hai wasiwe
hai tena kwa ajili ya nafsi zao wenyewe, bali kwa ajili yake yeye aliyekufa
akafufuka kwa ajili yao (2 Kor 5:14,15).
Baadaye Zungumzieni Jambo Hili
Kufanya uinjilisti katika eneo
unakoishi hakuna shida, lakini umisheni unaanzia wapi kwako, na utendaji wake
unakuwaje? Je, unafikiria kwenda mahali?
Jambo La Kufanya Kabla Hatujakutana
Tena
Tafakari Zaburi ya 116 mstari kwa
mstari uone ni mambo mangapi aliyokutendea Bwana. Na kisha fanya uamuzi wa kuwa
mwaminifu kwake na kuomba.
Kazi Ya Kuandika Ya Stashahada
Angalia hatua za kuwafikia
waliopotea kama zilivyoainishwa katika Rum 10:14,15. Zitambue na kuzielezea kwa
maelezo ya kurasa mbili.
Tafakari Mistari Hii
Yn 1:40,41
Tumia Dakika moja Kuubadilisha Ulimwengu
Ombea
taifa la Ugiriki
Idadi ya watu: 10,000,000; Dini: Orthodox, Waprotestanti ni 2% tu.
1. Umisheni Ni Nini?
Kila mwamini anajua kwamba cho chote alichonacho katika maisha haya na milele yote ni mali ya Mungu. Wakati tulipokuwa wenye dhambi na kuwa machukizo mbele za Mungu, Mungu mwenyewe alitutafuta na kutukomboa kutoka kwa Shetani kwa damu ya Mwanaye; na sasa ametufanya wana katika familia yake, akitubariki baraka nyingi (Yn 1:16).
Mwandishi Wa Zaburi Anauliza Kwa Niaba
Yetu Sote
’Nimrudishie Bwana nini kwa
ukarimu wake wote alionitendea?’ (Zab 116:12). Jibu letu leo halitofautiani na
lile alilolitoa miaka mingi sana iliyopita, ‘Nitakipokea kikombe cha wokovu; na
kulitangaza Jina la Bwana’ (ms 13).
Hatua Inayofuata Ni Umisheni
Tukiwa na moyo uliojaa upendo na
shukrani kwa Yesu, tunakwenda hatua moja zaidi, ng’ambo ya eneo tulilozoea
kufanya uinjilisti; na kukiinua juu kabisa kikombe cha Mungu cha wokovu, ili
kila mtu akione hata miisho ya nchi, na wao pia watake kukinywea kikombe hicho
chenye maji ya uzima.
Biblia inasema kwamba tunapaswa kushuhudia Yerusalemu, ambayo ni mji wa nyumbani kwetu, kisha Yudea na Samaria ambayo ni miji na mikoa ya jirani, na kisha tuende hata miisho ya nchi.
Paulo anapowaandikia rafiki zake wa kanisa la Korintho huko Ugiriki anawapa sababu nyingine zaidi na nzuri za umisheni.
2. Kumcha Bwana Kunatuhamasisha
Kumcha Bwana, phobos, kuna maana ya kuwa na hofu ya kumwudhi Mungu kwa kutokutii amri zake, pamoja na unyenyekevu na upendo kwake ndiko kunakotuhimiza sisi kumtii Yeye (2 Kor 5:11).
3. Mahitaji Ya Watu Yanatuhamasisha
Tunapoona uovu ukiwa umewakamatia watu kwenye dhambi, magonjwa, kukosa haki, umaskini, kutokuamini, ubinafsi, na madhara yake yote, na mateso yanayosababishwa na uovu huo; mioyo yetu inataka tufanye kitu fulani; kwa sababu tunaufahamu wema wa Mungu na yale yote Yesu aliyotufanyia. Paulo anasema ni lazima tujaribu kuwashawishi watu kila mahali wapate kubadili misimamo yao wakubali kumfuata Yesu (2 Kor 5:11).
4. Tunasukumwa Na Upendo
Upendo kwa watu wote na kwa kujali hatima yao ndio uliompeleka Yesu Msalabani, na sasa upendo huo umeujaza moyo wa Paulo na kumfanya ashiriki katika mpango mkuu wa Mungu wa wokovu.
Nasi Pia Tunapaswa Kusukumwa Na Upendo
Tunapotambua kwamba Yesu alikufa
kwa ajili ya watu wote, nasi pia tunachagua kufa kwa kumpa maisha yetu na
mipango yetu kama shukrani zetu; na kuanza kuishi kwa ajili ya Mungu na kwa
ajili ya watu wengine po pote walipo (2 Kor 5:14).
5.Tunahamasishwa Na Umilele
Paulo anasema hatupaswi kuwatambua watu kwa mafanikio ya ulimwengu huu; tusiangalie cheo, wala utajiri, au nafasi ya mtu. Badala yake tuwaone kwa mtazamo wa kweli za kutisha za kaburi. Uchaguzi ni lazima ufanyike sasa kuhusu mahali pa kuishi milele kati ya mbinguni na jehanamu.
Je, Ni Kweli Watu Wamepotea?
Mtu wa kwanza, Adamu, kwa hiari
yake aliamua kutokumtii Mungu na kuchagua kufuata uongo wa Shetani. Mungu naye
akaamua kumwacha Adamu, na roho ya Adamu ambayo ndiyo iliyomjua Mungu ilikufa
ndani yake. Adamu akabakiwa na mwili na nafsi tu, huku akimfuata bwana mkatili
kifoni na kuelekea kwenye moto wa jehanamu ambao haukuandaliwa kwa ajili ya
mwanadamu bali kwa ajili ya Shetani na malaika zake (Mt 25:41).
Mwanadamu Bado Amefungwa…
…na ule uamuzi wa kijinga
uliofanywa na yule mwakilishi wetu na anatembea akiwa amepotea kuelekea kwenye
umilele wa waliopotea ambako panatisha sana na ubaya wa huko ukishaingia huwezi
tena kuukwepa na wala hauna mwisho. Kwahiyo Paulo alikuwa sahihi aliposema
kwamba sisi tumekufa katika uasi na dhambi zetu tukimfuata Shetani na kuingojea
hasira ya Mungu, mpaka hapo tutakapokuwa tumeokolewa na Mungu kupitia kwa Yesu (
Efe 2:1-3,5).
Kuokolewa Na Jehanamu
Neno la Mungu linasema kwamba mtu
hana budi kuwa kiumbe kipya; kilichozaliwa mara mbili; mara ya kwanza katika
mwili, na mara ya pili katika roho kwa uweza wa Roho Mtakatifu ( Yn 3:3-6).
6. Tunahamasishwa Na Injili
Wakati fulani tulimwona Yesu kwa namna ya kimwili, tukimwona yeye kama mwanadamu wa kawaida tu, aliyefanya historia kama watu maarufu waliopita. Lakini sasa tumegundua ya kwamba kwa kweli alikuwa ni Mungu mwenyewe aliyekuwa Msalabani na akiwa anaupatanisha ulimwengu na nafsi yake mwenyewe, asituhesabie tena dhambi.
Hizi ni habari nyeti kati ya habari zilizowahi kusimuliwa katika historia ya mwanadamu na zinadai kukubalika na kupata jibu. Tuna ujumbe wa ajabu kwamba yule asiyekuwa na dhambi alifanyika dhambi na kulipa bei yake, yaani mateso na kifo, ili kwamba sisi tuliostahili adhabu tuweze kufanyika wenye haki na kuishi katika uwepo wa Mungu sasa na hata milele (2 Kor 5:18,19,21). Katika Mdo 4:12 tunaambiwa kwamba hakuna jina jingine tulilopewa litupasalo kuokolewa, isipokuwa jina la Yesu.
7. Wito Wenyewe Unatuhamasisha
Paulo anasema sisi tu mabalozi wa mbinguni, tukimwakilisha Mungu mwenyewe; Naye amekuwa akinena na watu waliotuzunguka na ambao hawana amani Naye. Na kama vile mabalozi wa kidunia wakiwa kwenye ukanda wa vita, mtindo wetu wa maisha kama wajumbe wa Mungu katika eneo la adui Shetani ni hatari na jambo linalohitaji uangalifu mkubwa (2 Kor 6:3-10). Kupitia kwetu Mungu anawahimiza na kuwataka watu wapatanishwe na Baba wa Mbinguni mwenye upendo.
Siku Iliyokubalika Ni Leo
Wakati uliokubalika ni sasa.
Kama si wewe, ni nani?
Na kama si sasa, ni lini?
(2 Kor 5:20 – 6:2)
Kwahiyo unaweza kuona kwamba kwa kumcha Mungu, mahitaji ya wanadamu, upendo wa Mungu, na kweli za umilele; habari nyeti tulizonazo za kusimulia, na wito wa Mungu, ni sababu tosha tulizonazo za kuchangia shughuli za umisheni; ikiwa ni karibu au mbali, ikiwa tunakwenda kwa maombi au kwa kutoa, ikiwa tunasafiri wenyewe au tunatuma mtu mwingine.
Kwa Kumalizia Omba Kwa Ajili Ya Watu Wa Ulimwengu Huu Ambao Bado Hawajafikiwa Na Habari Njema
Cameroon |
||
Jina La Watu |
Lugha Yao |
Idadi Yao |
Mada |
Mada |
17,000 |
Ngossi (Gevoko) |
Gevoko |
20,000 |
1985 - 2007
With many thanks to Pastor Dastan
Mboera, Dar es Salaaam, Tanzania
and EAPTC Nairobi, Kenya for this revision and translation from the original
English.
mboeradsk @ yahoo.com
© Dr Les Norman The DCI Trust, UK
Permission is
granted to provide copies at cost price for study purposes
but not for
sale or commercial purposes. Freely you have received, so please freely give.
Support Pages
Index to All Lessons School of Finances
World Christian News
Who
Are We? Site Index
www.dci.org.uk