1985 - 2007

 

18. Kuwafikia Wasiofikiwa Bado

Watu wa mwisho kabisa ambao hawajafikiwa ni wale wanaozuiwa na siasa au dini

Support Pages   Index To All Lessons   School of Finances  
World Christian News   
Who Are We?   Site Index
 

Katika Biblia Yako Soma
Zaburi 139;  Mithali 8.

Mstari wa Kukariri
Panua mahali pa hema yako, na wayatandaze mapazia ya maskani yako; usiwakataze; ongeza urefu wa kamba zako; vikaze vigingi vya hema yako. Kwa maana utaenea upande wa kuume na upande wa kushoto; na wazao wako watamiliki mataifa; wataifanya miji iliyokuwa ukiwa kukaliwa na watu (Isa 54:2, 3).

Baadaye Zungumzieni Jambo Hili
Tazama ramani ya watu wasiofikiwa bado ili kuona mahali walipo. Je, ni akina nani hao? Je, wako jirani au mbali nawe? Je, bila fedha unaweza kuwaendea au la?

Jambo la Kufanya Kabla Hatujakutana Tena
Zungumza na mchungaji wako au wazee wa kanisa kuhusu uwezekano wa kanisa lenu kuanzisha utaratibu wa kuombea kundi la watu ambao hawajafikiwa bado, kufanya utafiti na pengine kwa neema ya Mungu watu hao waweze kufikiwa na timu kutoka kanisani kwenu.

Kazi Ya Kuandika Ya Stashahada
Fikiria kwamba unaishi katikati ya kundi la watu ambao bado hawajafikiwa. Wewe ni nani, na unaamini nini? Hofu yako kubwa ni nini? Andika kurasa mbili.

Tafakari Mstari Huu Neno Kwa Neno
Yer 8:20

Tumia Dakika Moja Kuubadilisha Ulimwengu

Ombea taifa la Tajikistan

Idadi ya watu: 6,300,000  

Waislamu ni 82% ; Kuna Wakristo wachache tu;  Na watu wengi hawajafikiwa.

 

Fanya Rejea Ya Masomo Yafuatayo

16. Kumaliza Kazi
Kuliandaa kanisa kwa ajili ya Agizo Kuu, kufungua maudhui ya mataifa ambayo hayajafikiwa.

17. Watu Wasiofikiwa Bado
Jinsi ulimwengu unavyoonekana, kwa mtazamo wa kimbingu.

74. Kanisa La Kimishenari
Kuuingia ulimwengu wa umisheni, na namna ya kuanza.

Pengine ni mara ya kwanza umewezeshwa kuelewa kuhusu mataifa ambayo hayajafikiwa; na hapa mataifa ina maana ya makundi ya watu waliounganishwa na lugha moja, historia moja, au utamaduni mmoja. Unajua kwamba Yesu hawezi kurudi mpaka haya mataifa yawe na kanisa la kitaifa linaloweza kushuhudia watu wake, hata kama kanisa hilo ni dogo kiasi gani!

Kwa Hao Waliopewa Vingi, Kwao Vitadaiwa Vingi
Haya ni maneno ya Yesu katika Lk 12:48.

Kanisa La Magharibi Limepewa Vingi
Kwa sababu kanisa katika nchi za Magharibi limepewa vingi kwa maana ya nuru, maono, na mali, vingi vitadaiwa kutoka kwao. Si mpango wa Mungu kwamba waamini waingie katika maisha ya starehe kabla watu wa ulimwengu wote hawajapata fursa ya kusikia habari za upendo wa Mungu na wokovu.

Makanisa Ya Karismatiki Ni Zaidi
Kwa kuwa makanisa haya yamepokea vingi kwa maana ya uwepo wa Roho Mtakatifu na karama zake, vingi vitadaiwa kutoka kwao. Si mpango kamili wa Mungu kwamba waamini na wachungaji wao watumie muda mrefu daima wakiogelea katika upako wa Roho Mtakatifu, baraka na karama zake, kwa manufaa binafsi tu wakati sehemu tu ya huu uweza wa Roho ukitumiwa kwa usahihi unaweza kupeleka injili kwa watu wasiofikiwa bado na ambao wanaweza wakapotea milele.

Viongozi Wa Kanisa Wamepewa Vingi Zaidi
Kwa vile viongozi wa makanisa ya nchi za Magharibi na katika ukanda wa uamsho ulimwenguni kote wamepewa watu wengi na fedha, Bwana atadai vingi kutoka kwao. Kamwe si mpango mkamilifu wa Mungu kwamba nguvu nyingi itumike katika mashindano baina ya makanisa katika kujenga mahekalu makubwamakubwa na makundi makubwa ya wakristo wa majina wanaovutwa na vipindi vya burudani, wakati wanaume na wanawake wanaendelea kuangamia milele kwa kukosa kuisikia injili angalao mara moja.

Kwahiyo kwa sehemu kubwa , ni makanisa ya Magharibi na yale ya karismatiki na viongozi wao ndio wenye wajibu mkubwa wa kuwezesha kukamilika kwa Agizo Kuu katika kizazi chetu. Ingawa kazi kubwa inaweza kufanywa kwa uzuri zaidi na makanisa ya nchi zinazoendelea ambayo yako karibu zaidi na walengwa, yanahitaji kwa haraka maombi, mafunzo, na msaada wa fedha, ambazo zinaweza kupatikana kutoka makanisa yenye nguvu ya Magharibi. Na kwa ule mfano wa talanta, kama watumishi hawatumii karama wataipoteza (Mt 25:14-30).

Je, wasiofikiwa wanawezaje kufikiwa hata na kanisa la watu wasiokuwa na uzoefu, lakini wana moyo wa kufanya hivyo, na hawana kitu kikubwa cha kutoa? Mpango Wa Yoshua Wa Mwaka 2000 BK unaoratibu kazi miongoni mwa mataifa yaliyobakia kufikiwa unatupatia hatua rahisi zifuatazo:

1. Kwanza Ainisha Mataifa Ambao Hawajafikiwa
Kwa kutumia anwani hii ya Mradi Wa Yoshua http://www.joshuaproject.net/index.php unaweza kupata taarifa muhimu na za karibuni kabisa kuhusu maeneo ya dunia yenye watu ambao hawajafikiwa na injili. Utawajua ni akina nani, ni mahali gani walipo, na ni nani, kama yupo, anayejaribu kuwafikia. Unaweza kuagiza vipeperushi kwa kila kundi la watu kutoka kwa Bethany Prayer Centre kwa kupitia anwani ya Mradi Wa Yoshua. Ndani ya maktaba ya http://www.dci.org.uk/ kuna Kitabu Cha Anwani ambapo misheni nyingi zimeorodheshwa.  Waweza pia kufungua tovuti hii http://www.missionfrontiers.org/ kwa msaada zaidi.

2. Pata Watu Wenye Mawazo Kama Yako Kanisani Au Kwenye Internet
Kazi hii si rahisi kwa mtu mmoja, au kwa kanisa au kwa dhehebu. Ufumbuzi ni kwa makanisa ya nchi za Magharibi kuwasiliana na nguvukazi ya makanisa ya uamsho ulimwenguni kote, na kwa pamoja wawasiliane na makanisa yasiyokuwa na uwezo lakini ambayo yako jirani na watu ambao hawajafikiwa. Na kwa pamoja wawe na mkakati wa maombi, watu, fedha, vifaa, na hekima.

3. Kipekee Fanya Utafiti Kuhusu Mataifa Uliochagua Kuwaendea
Zaburi  8:4 inauliza swali, “Mwanadamu ni nani?” Tunapaswa kuwafahamu vizuri watu tuliochagua kuwaendea, kwahiyo tunarudi tena kwenye tovuti ya Mradi Wa Yoshua http://www.joshuaproject.net/index.php na kisha kwenye maktaba yako, na ensaiklopedia iliyoko kwenye mtandao wa internet. Taarifa za maelfu ya mataifa (ethnos) zinapatikana humo.

4. Anza Kuwafahamisha Watu Kinachoendelea
Ukiisha kuchagua mataifa unaokusudia kuwaendea ni muhimu kulifahamisha kanisa lako lote na makanisa mengine ya ndani ya nchi, pamoja na waratibu wa kimataifa ili wajue unachokusudia kukifanya, ili kwamba ushirika uandaliwe, na pia kuepuka uwezekano wa kazi moja kufanywa na timu mbili badala ya moja. Kutoa taarifa kama hizi ni muhimu kwa ajili ya maombi, kuhamasishwa, na kuwekwa mkakati.

5. Maombi Yako Yatafungua Njia
Unaweza kufanya maombezi kwa ajili ya watu walioko katika dirisha la 10/40 ukiwa nyumbani kwako na katika nchi yako. Wakati mwingine watu wa huduma ya AD2000 na YWMA huratibu maombi ulimwengu mzima kwa malengo maalum, mathalani kwa ajili ya Wahindu. Kutembelea maeneo kwa ajili ya kufanya maombi, wakati mwingine kimyakimya na kutokuvuta watu ikiwa ni lazima, kwafaa sana maana kunaweza kulibadili taifa.

6. Hatua Inayofuata Ni Kwa Kanisa Kuchagua Taifa (ethnos)

  1. Kwa pamoja, ombeni ili kupata maelekezo kuhusiana na watu mliowachagua.
  2. Kwa pamoja, mfahamishane, na kuwafahamisha wengine kwenye kanisa kuhusu kinachoendelea.
  3. Kwa pamoja, mjadili na mchungaji wenu, na kumpa fursa ya kujua yale mnayokusudia kuyafanya.
  4. Fanya maamuzi na kikundi cha misheni, kama hakipo ni vema kiundwe ili kusimamia kanuni.
  5. Wasiliana na uongozi wa kanisa kwa kila hatua unayoifanya.
  6. Wasiliana na mawakala wa umisheni au kanisa la kitaifa lililo jirani nawe ambao wanaweza wakawa na mipango ya kuwafikia watu hao. Kama hawana mpango, kufika kwako kunaweza kuwa ni msaada kwao kwamba wakati umewadia kwa kazi hiyo kufanyika.
  7. Omba tea na tena mpaka umeona njia sawasawa, na katika umoja, na kwa neema ya uvumilivu. Jiandae kwa mapambano ya vita vya kiroho, mkifunga nguvu za giza zilizowatawala watu hao kwa muda mrefu, na kufungulia uweza wa Roho Mtakatifu na uwepo wa malaika. Panga muda wa maombi wa mara kwa mara, utakaojulikana na kufuatwa na wanamaombi wote.
  8. Chagueni lile taifa atakalowachagulia Mungu, na mnalifahamu.
  9. Ombeni kwa ajili ya mkakati wa Mungu wa kuwafikishia injili taifa mlilolichagua ama, ama kwa kupitia kwenu, au kwa wakala au kwa waamini  walioko ndani ya nchi.
  10. Fanya mawasiliano ya mara kwa mara kuhusu maono yako na shughuli unazozifanya, na kanisa, makanisa ya jirani, Mradi Wa Yoshua, Makao Makuu ya dhehebu lako-kama lipo, mawakala wa umisheni, na makanisa yaliyoko jirani na taifa husika.

7. Lengo Ni Kupanda Kanisa
Taifa haliwezi kufikiwa mpaka pawepo na uwezekano wa kanisa lililojitosheleza, na la watu walio tayari kushuhudia. Zipo njia nyingi za kufanikisha jambo hili, lakini kwa vyo vyote vile mtu asijaribu kwenda mstari wa mbele bila mshirika (mbia) wake, ushauri, na msaada. Vitu muhimu vya kutilia mkazo katika mpango wa muda mrefu ni masuala ya uongozi, kujipanga vizuri, malengo, utafiti, kupima kazi, ushauri na kanisa la kitaifa lililoko jirani, kufanya umiliki wa pamoja wa mpango wa mwisho, kushirikisha wengi, kushirikiana kwa pamoja kwenye eneo la umisheni, na kufanya tathmini. Vitabu vingi vyenye ushauri mzuri na uzoefu vinapatikana kutoka AD2000 na Kituo cha Kimarekani cha Umisheni kinachoweza kupatikana kwenye mtandao kwa kutembelea tovuti hii: http://www.missionfrontiers.org/

Kujua La Kufanya Ni Muhimu Kwako

Unaweza ukakatishwa tamaa na ukubwa wa changamoto hii, lakini kushiriki kwako binafsi kunaweza kukawa ni kichocheo kinachoweza kufanya mambo yatendeke, na ukawa sababu ya taifa kufikiwa na injili ya Yesu. Kama asemavyo Isaya, “…usiwakataze; …Panua mahali pa hema yako, …enea upande wa kuume na upande wa kushoto”. 

 

Kwa Kumalizia Omba Kwa Ajili Ya Watu Wa Ulimwengu Ambao Hawajafikiwa Na Injili,Ukiwataja Kwa Majina

  

 

China (3)

Jina la Watu

Lugha Yao

Idadi Yao

Miao, Luobohe

Miao, Luobohe (2nd dialect)

60,000

Miao, Mashan Central

Miao, Mashan Central

70,000

Miao, Mashan Northern

Miao, Mashan Northern

35,000

Miao, Mashan Southern

Miao, Mashan Southern

10,000

Miao, Mashan Western

Miao, Mashan Western

14,000

Miao, Qiandong Eastern (Hmu Eastern)

Miao, Qiandong Eastern

350,000






 1985 - 2007

With many thanks to Pastor Dastan Mboera, Dar es Salaaam, Tanzania
and EAPTC Nairobi, Kenya for this revision and translation from the original English.
mboeradsk @ yahoo.com


© Dr Les Norman  The DCI Trust, UK
Permission is granted to provide copies at cost price for study purposes
but not for sale or commercial purposes. Freely you have received, so please freely give.

Support Pages   Index to All Lessons   School of Finances  

World Christian News   
Who Are We?   Site Index

www.dci.org.uk