1985 - 2007
20. Kutafuta Msaada
Support Pages
Index To All Lessons
School of Finances
World Christian News
Who
Are We?
Site Index
Katika Biblia Yako Soma
Wafilipi 1
Mstari Wa Kukariri
Maana najua ya kuwa haya
yatanigeukia kuwa wokovu wangu, kwa sababu ya kuomba kwenu, na kwa kuruzukiwa
Roho wa Yesu Kristo (Flp 1:19).
Baadaye Zungumzieni Jambo Hili
Thamani ya urafiki na maana yake
kwako. Je, unao marafiki wa karibu? Kama huna mwombe Mungu na baada ya muda
utaona yale atakayokufanyia.
Jambo La Kufanya Kabla Hatujakutana
Tena
Unaonaje ukiandaa tafrija nyumbani
kwako na kuwaalika rafiki zako na kuwafahamisha yale Mungu anayokuagiza na kile
unachokusudia kukifanya katika maisha yako. Tafuta marafiki na wala si
fedha,usiitaje hiyo.
Kazi Ya Kuandika Ya Stashahada
Fanya mazoezi kwa kuandika ukurasa
mmoja wa waraka ukiwaeleza rafiki zako na kanisa lako kile unachokifanya.
Waeleze unachokifanya na kwanini unakifanya. Waambie unakotaka kwenda, lini , na
utakuwa na nani. Waambie namna utakavyofikia lengo lako na gharama zake.
Tafakari Mistari Ifuatayo
Ayu 16: 20,21
Tumia Dakika Moja Kuubadilisha Ulimwengu
Ombea taifa la The Pacific. Idadi ya watu: 28,000,000.
Wakristo ni 75%. Kuna makabila machache hawajafikiwa.
Katika kuitikia wito wa Mungu kuhusu Agizo Kuu, kwa vyo vyote utahitaji kutafuta namna ya kujikimu ama kwa kufanya kazi au kwa kutegemezwa na kanisa au huduma yako.
Angalia Sehemu ya Uchumi Wa Ufalme
Hapo utapata maelezo ya kutosha kuhusiana na namna ya kuweza kupata fedha na namna ya kuanza na kutekeleza Agizo Kuu.
Je, Itakuwaje Iwapo Kanisa Lako Litashindwa Kukutegemeza?
Si jambo la ajabu kanisa likishindwa kukutegemeza. Lakini hata ikitokea hivyo usijali kwa kuwa zipo njia nyingine ambazo pengine zaweza kuwa bora zaidi kuliko kupokea cheki kutoka kwa mweka hazina wako.
Watu Wanahitajiana
Iwapo utaamua kuchangisha fedha, vema , utapata fedha kwa ajili ya matumizi. Lakini iwapo badala yake utaamua kutafuta marafiki, utapokea kutoka kwao upendo, watakuombea na kukushauri. Hekima yao na urafiki wenu waweza kudumu kwa muda mrefu na ukawa baraka kwako. Wakati mwingine fedha zinaweza kuwa na thamani ndogo kuliko marafiki. Soma habari za Paulo katika Wafilipi mlango wa kwanza.
Somo Kutoka Kwa Mungu Kwa Mambo Ya
Asili
Mfano: Fikiria kuhusu mti uliokua
na kusimama imara. Kumbuka kwamba chini ardhini mti huo una mtandao wa mizizi
iliyosambaa na kufika mbali kwa kazi ya kuusimamisha huo mti na kutafuta maji.
Hata upepo ukivuma, hata mvua kubwa ingenyesha, miti yetu inabaki imesimama.
Mtandao Wa Buibui
Sasa mtazame buibui. Utando wake uliosambaa unamwezesha kupata taarifa ya kiumbe cho chote kitakachosogelea. Buibui hukaa katikati ya mtandao imara aliousuka kwa ustadi. Makazi yake huyatumia pia kunasa chakula kwa ajili yake. Upepo ukivuma buibui huyo ataendelea kubaki salama salimini.
Kupata Marafiki ni Muhimu, Si Fedha Peke Yake
Huduma ya umishenari inatakiwa kuwa ya njia mbili, ya kwenda na ya kurudi. Huduma kwa ajili ya watu ambao hawajafikiwa ni ya muhimu sana; lakini usisahau kuwarudia wale waliokutegemeza. Watu hao wangependa washiriki binafsi katika zoezi hilo la umishenari lakini kwa sababu ya majukumu ya nyumbani, umri au udhaifu wanashindwa. Wewe unafanyika kuwa mikono yao, miguu yao, na midomo yao. Wangependa kuona unachokiona, kusikia unachosikia, na kuhisi unachohisi wewe. Hakikisha unawashirikisha.
Wanaokutegemeza Wanahitaji Kutegemezwa
Pia
Kumbuka kwamba si kila
anayekutegemeza ana kanisa linalomjali au hata mchungaji. Na upo uwezekano
kwamba mtu pekee anayewaombea na kuwajali ni wewe. Hakikisha unatimiza wajibu
wako mbele za Bwana.
Watendee Wengine Kama Ambavyo Wewe
Ungependa Kutendewa
Ikiwa utapanda mbegu za huruma,
fadhila, na kuwajali wengine, basi utarajie kuvuna yayo hayo. Zawadi ndogondogo
na postikadi ni muhimu hasa kwa wale watu wanaokaa nyumbani.
Kuna Mtu Mahali Fulani Anasubiri
Kusikia Kutoka Kwako
Watu siku hizi hawajali sana suala
la mawasiliano. Wanaonekana wako ‘bize’ kiasi kwamba hawana nafasi ya kutuma
wala kupokea habari. Wewe usiwe kama hao. Tuma postikadi yenye mistari michache
ya maneno ya kumtia moyo; wakumbuke katika matukio mbalimbali ya kukumbukwa kama
vile sikukuu ya kuzaliwa. Fanya mawasiliano kwa njia ya posta, simu, faksi,
barua pepe mesenja, na njia nyingine yo yote itakayokuwezesha wewe kuwasiliana
na rafiki zako na kuwaambia ‘asante kwa msaada wako’.
Mtazame Yesu
Hatuwezi kupuuzia umuhimu wa
rafiki zako. Kikundi cha watu sita au hata kumi na wawili kinaweza kuwa cha
thamani kubwa sana kwako kuliko ushirika mzima uliokusahau katika kipindi
kifupi. Nyuma ya kila mmoja wetu ipo neema ya Mungu, nawe unapaswa umtumaini
Yeye huku ukiishi maisha matakatifu na ya maombi. Pia uwe na imani na
kuzitazamia ahadi zake.
Utaanzia Wapi?
Jambo la kwanza, ni lazima uanze; ukikumbuka kwamba ishara zitakufuata, lakini ni mara chache sana zitakuja kama hujafanya lo lote kwa imani (Mk 16:17).
Waache Watu Wafahamu
Je, unakumbuka kufufuliwa kwa
Lazaro? Yesu alifanya ule mwujiza na watu wengi walihusika siku ile. Watembelee
watu majumbani kwao, na marafiki Mungu atakaokupa. Wafahamishe maono yako ili
upate kutoka kwao imani na maombi. Mungu anaweza kuwagusa wakakuuliza kama
utahitaji msaada wo wote wa kifedha wakati huo au baadaye. Vinginevyo uwe na
juhudi katika kutafuta marafiki; suala la fedha litafuatia baadaye. Watakapoamua
kukupa fedha ni lazima uwe na moyo wa shukrani kwa sababu wao ni neema ya Mungu
kwako.
Tambua Mahitaji Yako, Andaa Bajeti
Gawanya mahitaji yako ili kuufanya
mzigo kubebeka kirahisi. Kwa mfano: tuchukulie kwamba hitaji lako ni Sh. 10,000
kwa mwezi; unahitaji watu 10 watakaotoa Sh. 1,000 kila mmoja. Ni vyepesi zaidi
kuzungumzia Sh. 1,000 kuliko kuzungumzia Sh. 10,000 kwa mtu mmoja.
Tahadhari: Ulinde Sana ‘Mshipa Wako Wa
Fedha’!
Yule adui atapenda sana kuubana
mshipa wako wa fedha kwa sababu anajua akifanya hivyo mwendo wako kimaisha
utapungua sana. Chukua tahadhari kubwa kutokana na mashambulizi yake, na
usikubali kuanguka kwenye majaribu yake ya kukufanya uishi kiujanjaujanja, au
kukurudisha nyuma katika kumtolea Mungu kwa uaminifu. Anaweza akakujaribu katika
wito wako, au katika fedha, na pengine kukutegea katika kuchukuliana na watu
hata wale wasiofaa kwa sababu tu wana fedha. Mkaribie Mungu, wasamehe wale wote
wasiokuwa tayari kukusaidia; na sikuzote wafanye rafiki zako kuwa watu muhimu
kwako.
Kwa Kumalizia Omba Kwa Ajili Ya Watu Wa Ulimwengu Ambao Bado Hawajafikiwa Na Habari Njema Za Yesu
China | ||
Jina La Watu |
Lugha Yao |
Idadi Yao |
Wunai |
Bunu, Wunai |
13,000 |
Yang Huang |
T'en |
20,000 |
Younuo |
Bunu, Younuo |
13,000 |
Yung-Chuun |
Yongchun |
12,000 |
1985 - 2007
With many thanks to Pastor Dastan
Mboera, Dar es Salaaam, Tanzania
and EAPTC Nairobi, Kenya for this revision and translation from the original
English.
mboeradsk @ yahoo.com
© Dr Les Norman The DCI Trust, UK
Permission is
granted to provide copies at cost price for study purposes
but not for
sale or commercial purposes. Freely you have received, so please freely give.
Support Pages
Index to All Lessons School of Finances
World Christian News
Who
Are We? Site Index
www.dci.org.uk