1985 - 2007
21. Hatua Za Kwanza
Support Pages
Index to All Lessons
School of Finances
World Christian News
Who
Are We?
Site Index
Katika Biblia Yako Soma
Mdo 2:22-47
Mstari Wa Kukariri
"…Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa
jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha
Roho Mtakatifu (Mdo 2:38).
Baadaye Zungumzieni Jambo Hili
Je, nyote mmetubu, mmebatizwa,
mmempokea Roho Mtakatifu, na kujiunga na familia ya Mungu? Kama bado fanya
mipango sasa.
Jambo La Kufanya Kabla Hatujakutana
Tena
Andaeni orodha ya vitabu vya
kujifunza Biblia vinavyoweza kupatikana miongoni mwenu, au majumbani kwa waamini
wengine, na hata maktaba. Tafuteni vitabu vya itifaki, kamusi za Biblia, na vya
mafafanuzi na kamusi za lugha za zamani kwa mfano za Kiebrania na Kiyunani.
Vitawasaidia sana katika huduma.
Kazi Ya Kuandika Ya Stashahada
Chunguza ili kupata idadi ya
mabatizo ya maji katika Agano Jipya, na kisha andika taarifa ya kurasa mbili.
Tafakari Andiko Hili
Kol 3:1-10
Tumia Dakika Moja Kuubadilisha Ulimwengu
Ombea Saudi Arabia . Gharama ya kumfuata Yesu katika taifa hilo ni kifo. Karibu watu wote wapatao 17,000,000 ni Waislamu.
Katika Biblia Takatifu tunasoma jinsi Petro alivyowahubiri kundi kubwa la watu waliomkimbilia kuja kuona mwujiza wa waamini wa kwanza waliojazwa Roho Mtakatifu. Waliposikia habari za kuja kwa Yesu, Mwana wa Mungu na maisha yake, kifo chake kilichotokea mikononi mwa viongozi wao, kufufuka kwake na Ubwana wake mkono wa kuume wa Mungu, walimwuliza Petro swali muhimu sana ~
1. Je, Tufanyeje?
Jibu la Petro katika Mdo 2:38 linatujulisha mambo matatu muhimu ya kutuwezesha kujiunga na familia ya Mungu. Je, ni mambo gani hayo?
Tubu
Tunaweza tu kutubu
wakati Roho Mtakatifu anapozungumza na mioyo yetu nasi tukapata kufahamu madhara
ya dhambi zetu mbele za Mungu Mtakatifu. Kwa kweli tunajutia dhambi zetu na
kukiri na kisha tunatubu. Toba maana yake ni kugeuka nyuma na kuelekea huko
ulikogeukia. Tunatubu tunapoacha kutembea katika njia za dhambi za ulimwengu huu
na kuchagua kutembea katika njia za Mungu, na kumwomba atuwezeshe kufanya hivyo.
Ubatizwe
Petro alisema baada ya
toba, kila mmoja abatizwe kwa jina la Yesu Kristo kudhihirisha kwamba amepokea
msamaha wa dhambi zake. Ubatizo ni jambo la kimila ambalo walifanyiwa watu
walioamua kujiunga na imani ya Kiyahudi, kwahiyo watu waliokuwa wakimsikiliza
Petro walimwelewa. Lakini ubatizo wa wafuasi wa Yesu ulikuwa na maana zaidi ya
mila tu au sherehe. Ni kumfuata Bwana, ni mlango wa kuingilia katika maisha
mapya kwenye familia mpya.
Pokea Zawadi Ya Roho Mtakatifu
Hatuwezi kamwe kuishi
maisha ya ushindi bila uwezo na uwepo wa Roho Mtakatifu. Ni Yeye
anayeweza kumbadilisha mtu kutoka dini iliyokufa na kumfanya kuwa na uhusiano
ulio hai na Mungu. Tunamhitaji huyo atujaze maisha yetu na maisha ya waamini
wenzetu. Kumpokea Roho Mtakatifu maishani mwetu ni muhimu sana na Petro anasema
hilo ni moja ya mambo muhimu ya kwanza ya kufanya. Baada ya ubatizo tunapewa
Roho Mtakatifu tumnywe (1 Kor 12:13).
2. Yesu Mwenyewe Alibatizwa
Katika Mt 3:13-17 tunaweza kusoma habari za Yesu ambaye ni mfano bora wa maisha. Yeye alianza huduma yake baada ya kubatizwa.
Kubatizwa Kunadhihirisha Utii Kwa Yesu
Katika Mt 28:19 Yesu
aliagiza kwamba watu wabatizwe; na katika Yn 15:14 alisema sisi ni rafiki zake
kama tutazishika amri zake. Hebu soma pia Mdo 5:32.
Ni
Nani Abatizwe?
Katika Biblia tunaona
kwamba wanaobatizwa ni waamini pekee. Kila mwenye uwezo wa kuamini na abatizwe.
Je, Tendo La Ubatizo Linafanyikaje?
Neno ‘kubatiza’ katika
Biblia lina maana ya kuchovya au kuzamisha; kwahiyo ina maana waamini wa kwanza
walizamishwa ndani ya maji kwa muda mfupi, na kuibuliwa tena.
Ni Nini Kinachotukia Wakati Wa Ubatizo?
1. Ubatizo ni ungamo la hadhara la Imani mtu aliyonayo kwa Mungu kupitia kwa Yesu; na ni tamko kwa Mungu, kwa malaika, kwa mapepo, na kwa wanadamu kuhusu nia ya mwamini kumfuata Yesu (Mk 8:38).
2. Katika ubatizo mwamini anatambua kwamba Yesu alipokufa Msalabani utu wake wa kale ulikufa pamoja na Bwana. Dhambi zake zimeoshwa na sasa maisha ya zamani yanazikwa kama vile Yesu alivyokufa na kuzikwa. Mwamini anapoibuka kutoka majini anatambua na kwa imani anapokea maisha mapya akiwa ameunganishwa na Yesu katika nguvu ya ufufuo (Rum 6:3-6).
3. Ubatizo ni tamko la mwamini kwamba anajiunga na familia ya watu wa Mungu (1 Kor 12:12,13).
Je, Ni Lini
Mwamini Abatizwe?
Mapema iwezekanavyo.
Katika Mdo 2:38 wale watu walibatizwa siku ileile walipomwamini Yesu. Ubatizo ni
namna ya kupokea neema ya Mungu, na mwamini mpya anaihitaji neema hiyo mwanzoni
anapookoka ili imwezeshe kusimama.
3. Karibu Kwenye Familia Ya Mungu
Unapoamua kumfuata Yesu kwa kweli unajiunga na familia kubwa. Haiwezekani ukamfuata Yesu na huku unajifanyia mambo yako tu. Ni muhimu sana ufanyike sehemu ya familia ya Mungu, yaani kanisa lake. Utagundua kwamba kujiunga na kanisa kunaleta usalama na uimara katika maisha.
Je, Mwamini Ajiunge Na Kanisa Lipi?
Siku hizi kuna
makusanyiko mengi ya waamini; mengine ni ya kizamani, na mengine ni ya kisasa;
lakini kanisa zuri ni lile lenye sifa kama zile zilizoonekana katika kanisa la
kwanza, yaani kanisa la Agano Jipya (Mdo 2:42-47).
· Kudumu katika mafundisho ya mitume, ambayo leo hii tunayo katika Biblia. Mambo ya kwanza kabisa tunayopaswa kujifunza ni toba, imani kwa Mungu, mabatizo, kuwekea mikono, ufufuo wa wafu, na hukumu ya milele (Ebr 6:1,2).
· Kudumu katika urafiki wa kweli.
· Kudumu katika kupokea neema ya Mungu katika kumega mkate.
· Kudumu katika maombi.
· Kulikuwepo pia heshima na ibada mbele za Mungu, miujiza na waamini kuongezeka. Watu walishirikiana mali zao, walisaidia maskini, na walikusanyika ili kumtukuza Mungu majumbani mwao na hekaluni.
Lakini kumbuka kwamba toba, kubatizwa, kujazwa Roho Mtakatifu na kujiunga na familia ya Mungu, ni mwanzo tu wa mambo. Yapo mengi zaidi ya kugundua.
Kwa Kumalizia Omba Kwa Ajili Ya Watu Wa Ulimwengu Ambao Hawajafikiwa Na Injili
Misri | ||
Jina La Watu |
Lugha Yao |
Idadi Yao |
Albanian (Shqip) |
Albanian, Tosk |
18,000 |
Dom Gypsy (Nawar, Ghagar, Helebi) |
Domari |
234,000 |
Waarabu wa Libya |
Kiarabu, Kibedawi cha K/Mashariki |
300,000 |
1985 - 2007
With many thanks to Pastor Dastan
Mboera, Dar es Salaaam, Tanzania
and EAPTC Nairobi, Kenya for this revision and translation from the original
English.
mboeradsk @ yahoo.com
© Dr Les Norman The DCI Trust, UK
Permission is
granted to provide copies at cost price for study purposes
but not for
sale or commercial purposes. Freely you have received, so please freely give.
Support Pages
Index to All Lessons School of Finances
World Christian News
Who
Are We? Site Index
www.dci.org.uk