
1985 - 2007
32. Kufanana Na Yesu
Tunda la Roho ni asili ya Mwana wa Mungu
Support Pages
Index to All Lessons School of Finances
World Christian News
Who
Are We? Site Index
Katika Biblia Yako Soma
1 Yoh 3:1-3; Flp 2:1-11
Mstari wa Kukariri
Lakini tunda la Roho ni upendo,
furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, upole, kiasi; juu ya
mambo kama hayo hakuna sheria (Gal 5:22, 23)
Baadaye Zungumzieni Jambo Hili
Je, unaweza kuwaza kuhusu mtu ye
yote unayemfahamu, au kwa kuangalia kwenye historia, au kutoka kwenye vyombo vya
habari, anayeishi sikuzote maisha haya ya kufanana na Kristo?
Jambo La Kufanya Kabla Hatujakutana Tena
Tafakari kimyakimya maana ya
kibiblia ya kila neno katika haya: upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema,
fadhili, uaminifu, upole, na kiasi.
Jichunguze misimamo yako mwenyewe na uone jinsi unavyoweza kufikia
viwango vya juu kwa msaada wa Mungu.
Kazi Ya Stashahada
Andika aya tisa fupifupi ukionesha
kutoka kwenye vitabu vya Injili mahali Yesu alipoonesha tunda la Roho
Tafakari Andiko Hili
2 Pet 1:3, 4
Tumia Dakika Moja Kuubadilisha Ulimwengu
Ombea taifa la Austria. Idadi ya watu ni 8,000,000. Asilimia
83% ni Wakatoliki. Kuna tatizo kubwa la uchawi, ulevi, na watu kujiua.
Mungu anafanya kazi kubwa kuachilia ndani yetu tunda la Roho Mtakatifu, ambalo ni asili njema ya Yesu. Je, ni aina gani ya tunda analolitafuta katika maisha yetu?
1. Upendo, Lakini Wa Aina Gani?
Kuna aina nyingi za upendo kwa mfano kwenye Biblia tunakuta upendo wa familia au marafiki, upendo wa kuwa wa kwanza, upendo wa ndugu na dada, kupenda fedha, upendo wa mwanamke kwa familia yake, upendo wa mwanadamu na kupenda raha. Aina zote hizo ni za upendo wa kibinadamu, unaojulikana kama phileo. Lakini upendo mkuu wa Mungu una jina lingine, nalo ni agape. Anakupenda bila masharti, upendo wake hauongezeki wala kupungua kutokana na kushindwa au kushinda kwako. Anakupenda tu basi.
Mungu mwenyewe ni agape! (1 Yoh 4:8)
Kwa upendo huo alimpenda Yesu (Yn 17:26)
Mungu anawapenda watu kwa namna ileile na anaonesha upendo huo kwa kutoa zawadi ya Mwanaye (Yn 3:16) (1 Yoh 4:9, 10)
Baba anayo agape kubwa zaidi kwa wale wanaompenda Mwana wake Yesu (Yn 14:21)
Upendo Wa Agape Ukitenda Kazi
Wakati tulipokuwa bado wenye dhambi Kristo alitufia. Huo ni upendo wa agape (Rum 5:8).
Ona jinsi Yesu alivyoonesha kwa ukamilifu upendo wa agape katika Yn 13:1-34.
Yesu alituamuru kupendana, upendo wa agape, sisi kwa sisi, na kuwapenda watu wengine wote kwa upendo huohuo (Yn 13:34, 35) (1 The 3:12) (1 Kor 13:1-8).
Je, Maisha Yako Ya Upendo Yakoje?
Je, unalazimika kwenda ukisukumwa na agape? (2 Kor 5:14-20)
Jambo la kufanya na agape (1 Yoh 3:16-18)
Mahali pengine pa kupata agape (Rum 5:5).
2. Furaha, Ya Bwana
Yesu amepakwa mafuta ya furaha (Ebr 1:9). Yesu alifurahia watu, harusi, na tafrija. Neno katika Lk 10:21 aliruka kwa furaha, na kwa kuiona furaha mbele kulimsaidia Yesu kustahimili Msalaba (Ebr 12:2).
Kumfuata Yesu Kunaleta Furaha
(Lk 10:17) (Mdo 13:52)
Miji inaweza kupata furaha (Mdo 8:8)
Furaha ni lengo mojawapo la huduma (Flp 1:25) (2 Kor 1:24).
Yesu anataka uwe na furaha tele. Ukitaka kujua ni kwa namna gani, soma kutoka Yn 15:1-11).
3. Amani, Kama Mto
Maneno ya Biblia eirene na shalom yana maana ya utulivu katika taifa; hakuna vita hata baina ya mtu na mtu, kuna usalama, kuna kustawi, na furaha. Nafsi ya mtu aliyeokolewa ina amani na haihofii lo lote kutoka kwa Mungu, imeridhika na maisha, na imehakikishiwa uzima wa millele. Yesu ndiye Mfalme wa amani, naye huwapa amani watu wasiokuwa nayo. Hatushangai basi ni kwanini Paulo huanza nyaraka zake kwa maombi ya amani, eirene (Isa 9:6) (2 The 3:16) (Lk 7:50; 8:48).
Jinsi Ya Kuipata
Amani Ya Mungu
Kutokana na ahadi ya Flp 4:1-7
mahusiano yanakuwa mazuri.
Mtindo wa maisha wa kusifu katika mazingira yote.
Jua kwamba Bwana yu karibu kukutana nawe.
Usihofu, badala yake omba na kumwuliza Mungu.
Amani yake itaulinda moyo wako na ufahamu wako.
4. Nipe Uvumilivu, Sasa!
Hapa kuna neno makrothumia lenye maana ya ustahimilivu mwingi, uvumilivu, na uwezo wa kuzuia hasira yako kwa muda mrefu unapochokozwa. Neno hilo lina maana ya ustahimilivu tunaokuwa nao tunaposubiri kwa muda mrefu tukiwangojea watu wenye mioyo migumu waje kwa Kristo. Mungu naye anastahimili kwa muda mrefu wakati tunapochelewa kumjua (Rum 2:4; 9:22)
Kwa Imani, Na Kwa Uvumilivu
Tunapokea ahadi za Mungu (Ebr 6:12).
5. Fadhili Na Utuwema
Hapa kuna maneno mawili yanayofanana; chrestotes lenye maana ya utu wema katika kuhurumia, na la pili ni agathosune lenye maana ya kulifanyia kazi jambo lililo jema.
Yesu Alikuwa Mwema Na Alifadhili
Yeye alikuwa chrestotes, alionesha utu wema na huruma kwa yule mwanamke mwenye dhambi lakini aliyekuwa tayari kutubu. Lakini pia aliweka utu wema, agathosune, kwenye matendo alipolitakasa hekalu (Lk 7:37-50) (Mt 21:12, 13). Soma Mdo 10:30 ili uone vitu viwili vilivyosababisha Yesu atiwe mafuta.
6. Uaminifu
Yesu aliwaahidi wanafunzi wake kwamba atawatangulia kwenda Galilaya. Alionesha uaminifu kwa kuitunza ahadi yake, na neno lenye maana hiyo ni pistis. Kwa maana katika kulitunza neno lake Yesu alilazimika kupitia Gethsemane, kwenda Msalabani, kaburini, kuzimu, Mbinguni, kufufuka na hatimaye Galilaya (Mt 26:32).
Mpango wa Mungu Ni Kukufanya Wewe Uwe mwaminifu
Je, unaposema, ‘ndiyo’ unamaanisha, ‘ndiyo’? (Mt 5:37)
Je, unazitunza ahadi zako? (Zab 15:4)
Je, Mfalme atakuita wewe ‘mtumwa mwema na mwaminifu’? (Mt 25:21)
7. Upole
Neno praotes lina maana ya upole na unyenyekevu kama ule wa Yesu, unaotufanya sisi kukubaliana na yale yote Mungu anayotufanyia kuwa mema, hata kama hatuyapendi. Yesu ni Simba wa Yuda, lakini pia ni Mwanakondoo wa Mungu, mpole na mnyenyekevu mbele za Baba. Wenye upole wamebarikiwa (Mt 5:5). Tunapaswa kujifunza kutoka kwa Yesu (Mt11:29).
8. Je, Waweza Kuwa Na Kiasi?
Kama jibu ni ‘hapana’ basi unahitaji egkrateia, yaani kuwa na kiasi, ndiyo kusema uwezo wa kuudhibiti mwili wako dhidi ya tamaa.
Yesu Alijua Kusema Hapana!
Ukisoma kutoka Lk 4:1-14 utaweza kuona jinsi alivyojidhibiti mwenyewe katika kipindi cha udhaifu.
Wakati Yesu alipokuwa na njaa, Shetani alimwambia tumia vibaya uweza ulionao kwa hitaji lako binafsi la chakula. Yesu: HAPANA!
Shetani alimjaribu Yesu kwa kumpa njia fupi na rahisi ya kuukwepa Msalaba. Yesu: HAPANA!
Shetani alipendekeza njia ambayo Yesu angeweza kujipatia umaarufu haraka walipokuwa juu ya kinara cha hekalu. Yesu: HAPANA!
Tunahitaji Msaada Wa Mungu Ili Tuweze Kuwa Na Kiasi
Kuteka nyara fikira (2 Kor 10:5).
Kuufuga ulimi (Yak 3:8) (Mdo 2:4)
Kuidhibiti miili yetu (1 The 4:4)
Kwa Kumalizia Omba Kwa Ajili Ya Watu Wa Ulimwengu Huu Ambao Bado Hawajafikiwa Na Injili, Ukiwataja Kwa Majina
|
India |
||
|
Jina la watu |
Lugha yao |
Idadi yao |
|
Multani (Siraiki Hindi) |
Siraiki |
20,000 |
|
Muria (Jhoria) |
Muria, Western |
12,900 |
|
Nahari |
Nahari |
19,000 |
|
Panika |
Pamika |
30,700 |
|
Pao |
Pao |
23,500 |
|
Saharia (Sor) |
Saharia |
174,300 |
|
Sondwari |
Sondwari |
31,500 |

1985 - 2007
With many thanks to Pastor Dastan
Mboera, Dar es Salaaam, Tanzania
and EAPTC Nairobi, Kenya
for this revision and translation from the original English.
mboeradsk @ yahoo.com
© Dr Les Norman The DCI Trust, UK
Permission is granted to provide
copies at cost price for study purposes
but not for sale or commercial
purposes. Freely you have received, so please freely give.
Support Pages
Index to All Lessons School of Finances
World Christian News
Who
Are We? Site Index
www.dci.org.uk