1985 - 2007
34. Kuwekea Mikono
Ee Bwana, tujaze na Roho wako hadi kufurika
Support Pages
Index to All Lessons School of Finances
World Christian News
Who
Are We? Site Index
Katika Biblia Yako Soma
Kum 34
Mstari Wa Kukariri
Na Paulo, alipokwisha kuweka
mikono yake juu yao, Roho Mtakatifu akaja juu yao; wakaanza kunena kwa lugha, na
kutabiri (Mdo 19:6).
Baadaye Zungumzieni Jambo Hili
Je, kanisani kwenu kuna kuwekeana
mikono? Je, hilo ni jambo la kawaida kwenu au hutukia mara chache tu kwa mfano
mnapotembelewa na Askofu?
Jambo La Kufanya Kabla Hatujakutana
Tena
Kwa kibali cha viongozi wenu,
andaeni utaratibu wa kuwekewa mikono kila mmoja wenu ili mpokee uwezo wa
kuhudumu, baraka na uponyaji.
Kazi Ya Kuandika Ya Stashahada
Andika taarifa ya kurasa mbili
ukielezea ni lini kila tendo la kuwekea mikono lilifanyika na sababu zake.
Tafakari Mistari Hii Neno Kwa Neno
Kut 31: 1-6
Tumia Dakika Moja Kuubadilisha Ulimwengu
Ombea nchi zilizokuwa Yugoslavia ya zamani – yaani Serbia, Montenegro,
Bosnia, Croatia, Kosovo, Macedonia, na Slovenia. Kuna mateso na matatizo ya kikabila. Kuna wafuasi wachache wa madhehebu ya Kiinjili, lakini wanaongezeka.
Katika Ebr 6:1,2 mwandishi anataja mambo sita ya msingi ambayo kila mwamini mchanga anapaswa kuyajua, kabla hajaendelea kuukulia wokovu.
Kuwekea mikono ni mojawapo, na ndiyo maana utaona mara kwa mara watu wakiwekewa mikono katika mikutano ya maombi na kanisani. Maelezo kuhusu misingi mingine utakutana nayo kadiri tunavyoendelea na mafunzo yetu.
1. Kuwekea Mikono Ni Nini?
Unaweza kusema kwamba kuwekea mikono ni huduma ya mtu mmoja kwa mwenzake inayofanyika wakati mtu mmoja anapoweka mkono wake mmoja au yote miwili juu ya mwili wa mtu mwingine kwa kusudi maalum la kiroho. Kwa kawaida mtu anayewekewa mikono atakuwa anaombewa, au kutabiriwa wakati huohuo. Wakati mwingine kikundi cha waamini kitakuwa kimemzunguka mtu mwenye hitaji na kumwekea mikono.
2. Jambo Hili Linapatikana Wapi Kwenye Biblia?
Kwa hakika , kuwekea mikono ni jambo la baraka na la zamani sana linalojulikana na watu wa Mungu. Zipo kumbukumbu za matukio hayo tangu mwanzo wa nyakati.
Kutenga Kwa Ajili Ya Kifo
Katika Agano la Kale Wana wa
Israeli waliweka mikono yao juu ya vichwa vya wanyama kabla hawajachinjwa na
hatimaye kuchomwa ili kuhamishia dhambi zao kwa wanyama hao wanapotolewa kafara
(Kut 29:10, 15, 19, 29) (Law 1:1-5; 4:15; 8:4; 8:18, 22; 16:21; 24:14) (Hes
8:12) (2Nya 29:23).
Kuhamishia Baraka Za Kinabii
Yakobo alihamishia baraka za
mwisho za kinabii kwa wajukuu zake Efraimu na Manase, kwa maombi na kwa
kuwawekea mikono (Mwa 48:14).
Kumsimika Kiongozi
Musa alimwekea mikono msaidizi
wake Yoshua ili kuhamishia kwake mamlaka na hekima kama kiongozi mpya wa watu wa
Mungu (Kum 34:9) (Hes 27:15-23) (Yos 1:16, 17) (Hes 8:10) (Hes 27:23).
Kuhamishia Uponyaji
Yesu alihamishia uponyaji kwa
wagonjwa kwa kuwawekea mikono. Wazee wa kanisa humpaka mafuta mgonjwa, humwekea
mikono yao na kumwombea uponyaji. Waamini pia wanao uwezo wa kuhamishia uponyaji
kwa mgonjwa kwa kumwekea mikono (Mk 5:23; 6:5; 8:23-25; 16:18) (Lk 4:40; 13:13)
(Mdo 9:12-17; 28:8, 9) (Yak 5:14-16).
Kuhamishia Baraka
Yesu alipenda hasa kuhamishia
baraka za Mungu kwa watoto wadogo (Mt 9:13-15) (Mk 10:13-16).
Kuhamishia Amani
Yesu alimwekea Yohana mkono na
kusema, “Usiogope” (Ufu 1:17).
Kuhamishia Roho Mtakatifu
Waamini kwa ujumla, na viongozi,
walihusika katika kuwahamishia wengine ubatizo wa Roho Mtakatifu kwa njia ya
kuwawekea mikono (Mdo 8:14-24; 9:10-17; 19:6).
Kuhamishia Karama Za Kiroho
Karama za neema kutoka kwa Yesu
zilihamishwa na Roho wa Mungu kwa njia ya kuwekea mikono (1Tim 4:14) (2Tim 1:6)
(Rum 1:11).
Kutenga Wamishenari
Katika Mdo 13:1-4 Paulo na Barnaba
wanatengwa na kanisa kwa kazi ya umishenari kwa kuwekewa mikono, na hivyo
kupokea upako maalum kwa ajili ya huduma hiyo.
Kuwaingiza Kazini Watumishi Wa Kanisa
Kuingizwa kazini kwa wale viongozi
saba wa makanisa katika Mdo 6:1-6, kulihusisha pia kuwekewa mikono na mitume.
Watu hao saba tayari walikuwa waamini.
3. Je, Ni Lini Mtu Awekewe Mikono?
Ni lazima pawepo na muda wa kutosha wa kumfahamu, na kila tahadhari ichukuliwe kabla ya kumwekea mikono mfanyakazi mpya wa kanisa, mchungaji au mmishenari. Kuwekea mikono ni jambo la mwisho kabisa na la hadhara katika mchakato mzima wa kufanya maamuzi mbele za Bwana. Ni wazi kwamba usingetaka kuchagua mtu mbovu, ambaye baadaye angeweza kusababisha uharibifu na mgawanyiko kanisani (1Tim 5:22).
4. Ni Nini Kinachotokea Wakati Wa Kuwekea Mikono?
Hapa hatuzungumzii kuhusu taratibu au sherehe zinazofanyika kanisani. Hizo ni sherehe za kuweka mikono mitupu juu ya vichwa vitupu. Zingekuwa ni sherehe zisizokuwa na maana na zinazokosa kibali cha Mungu. Wakati viongozi au waamini wanapomwekea mtu mikono ni kwa sababu wanataka Mungu aachilie Roho wake na neema yake kupitia mikono hiyo wakati wa huduma inayoongozwa na Roho Mtakatifu (Kum 34:9).
Uwe Mwangalifu Ni Nani Anayekuwekea
Mikono
Kwa sababu uhamisho unaofanyika
wakati wa kuwekea mikono ni halisi, na wenye uweza mkubwa; na kwa sababu si Roho
Mtakatifu peke yake anayeweza kuhamishwa, ni lazima uchukue tahadhari ni nani
unayemruhusu akuwekee mikono yake. Usimruhusu kukuwekea mikono mtu
anayejihusisha na mambo ya kichawi na ushirikina, au anayetenda dhambi kwa
kukusudia; kwa sababu upo uwezekano wa mtu huyo kukuhamishia pepo mchafu na
akakusumbua maishani mwako.
Mwulize Mungu kimoyomoyo katika maombi, kama alivyofanya Nehemia katika Neh 2:4 na kwa haraka tathmini tabia ya mtu anayetaka kukuwekea mikono. Kama ukikosa amani, basi unaweza kwa upole kabisa kukataa kuwekewa mikono.
5. Utawekeaje Mikono?
Isingeweza kurahisishwa zaidi kwa sababu unachopaswa kukifanya ni kukubali kuwa chombo cha baraka za Mungu kwa mtu mhusika. Roho Mtakatifu atafanya mengine yote kutokana na mwitikio wako wa upendo, utayari wako na maombi yako; na utayari na uwazi wa yule mlengwa.
Kwa Kumalizia Omba Kwa Ajili Ya Watu Wa Ulimwengu Huu Ambao Hawajafikiwa Na Injili, Ukiwataja Kwa Majina
Iran | ||
Jina la watu |
Lugha yao |
Idadi yao |
Aimaq, Jamshidi (Char Aimaq) |
Aimaq, Jamshidi |
30,000 |
Aimaq, Timuri (Teymur, Timuri) |
Aimaq, Taimuri |
181,000 |
Azerbaijani (Azeri) |
Azerbaijani, South |
22,000,000 |
Balkan Rom Gypsy |
Romani, Balkan |
24,000 |
Baluch, Southern |
Baluchi, Southern |
405,000 |
Baluch, Western |
Baluchi, Western |
29,000 |
1985 - 2007
With many thanks to Pastor Dastan
Mboera, Dar es Salaaam, Tanzania
and EAPTC Nairobi, Kenya
for this revision and translation from the original English.
mboeradsk @ yahoo.com
© Dr Les Norman The DCI Trust, UK
Permission is granted to provide
copies at cost price for study purposes
but not for sale or commercial
purposes. Freely you have received, so please freely give.
Support Pages
Index to All Lessons School of Finances
World Christian News
Who
Are We? Site Index
www.dci.org.uk