1985 - 2007

 

35. Mateso

Ni magumu, hata kwa Wakristo

Support Pages   Index to All Lessons   School of Finances  
World Christian News   
Who Are We?   Site Index
 

Katika Biblia Yako Soma
1Pet 4:12 – 5:11

Mstari Wa Kukariri
Lakini nawaambia, ‘Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi; ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki (Mt 5:44,45).

Baadaye Zungumzieni Jambo Hili
Mateso yenu wenyewe, na kisha mwombeane ninyi kwa ninyi, na kufarijiana kila mmoja na mwenzake.

Jambo La Kufanya Kabla Hatujakutana Tena
Watafute, wafariji, na kuwatia moyo watu wanaoteseka kwa umaskini,
kutengwa, magonjwa kama ukimwi, na walio kifungoni. Jipatie rafiki angalao mmoja kutoka kila kundi.

Kazi Ya Kuandika Ya Stashahada
Elezea kwa undani zaidi zile sababu tatu zinazosababisha kuwepo na mateso, na kisha uone kama unaweza kupata nyingine zaidi

Tafakari Mistari Hii
Lk 6:20-23

Tumia Dakika Moja Kuubadilisha Ulimwengu

Ombea taifa la Libya. Idadi ya watu ni 5,500,000. Asilimia

97% ni Waislamu; Asilimia 3% ni Wakristo wa mataifa ya nje. Hakuna injili ya waziwazi.

 

Mateso yanamgusa kila mmoja wetu na kwa wengine yanaweza kuendelea hata kwa miaka kadhaa kutokana na magonjwa, ajali, au kuumia kimawazo kunasababishwa na kukata tamaa na huzuni kubwa. Vifo, kukosa ajira, na usaliti ni vitu ambavyo kwa kweli vinatia uchungu vinapotokea kwenye ndoa, familia au kanisani. Umaskini nao huleta mateso kwa kusababisha ukosefu wa chakula, maji safi, na madawa. Kadhalika siasa au dini huweza kusababisha mateso makubwa kutokana na matumizi mabaya, kutotendewa haki, kukosekana usawa, na kutengwa.

1. Mungu, Uko Wapi?

Mateso ni halisi, na ili Mungu awe Mungu ni lazima awe Mwenyezi na hujidhihirisha mwenyewe kama Mungu wa upendo. Wanadamu wamekuwa wakipambana na hali hii kwa miaka mingi.

Mwandishi wa vitabu Steven Chalke Aliwahi Kuandika Haya:
" Pengine Mungu anataka kufanya jambo fulani, lakini anashindwa. Pengine kukomesha umaskini wa dunia ni kazi kubwa sana inayomshinda. Kama hivyo ndivyo, basi huyu si Mwenyezi. Pengine Mungu mwenyewe ni Mwenyezi, lakini hajali sana kukomesha mateso ya watu. Kama hivyo ndivyo, basi Mungu huyo hana upendo. Lakini pengine Mungu huyo anajali, na ni Mwenyezi, lakini kwa mtazamo wake wa muda mrefu haoni kama mateso na uovu ni halisi, au kuwa ni tishio kama sisi tunavyoona. Pengine haya yote ni sehemu tu ya mchakato wa mafunzo kabambe. Kama hivyo ndivyo, basi mateso na uovu si halisi.

Je, Kuna Jibu Lo Lote?
Watu wengine wanasema kwamba kupata mateso si jambo baya sana; wengine wanasema ni sehemu tu ya picha kubwa zaidi ya kutusaidia kujifunza; wengine wanasema ni matokeo ya dhambi za watu wenyewe; na wengine pia wanasema kwamba mateso yanasababishwa na Shetani katika vita vya kiroho. Majibu haya kwa pamoja yanaonekana kutoa sehemu tu ya maelezo, lakini hatuwezi kuelewa mpaka Yesu atakapotoa maelezo sahihi huko mbinguni.

2. Tunajua Sababu Tatu

Ulimwengu Uliopotoka

Kwanza,tunaishi kwenye ulimwengu uliopotoka, ambao umeathiriwa sana na dhambi kutoka anga za juu sana mpaka duniani, vitu vidogo sana na vya ngazi za atomiki na hii inakuwa ni sababu ya madhara ya hali ya hewa, maafa ya asili na matatizo ya kiafya katika miili yetu.

 

Hiari Ya Mwanadamu

Pili, hiari ya mwanadamu, ambayo ni uwezo aliopewa na Mungu wa kuchagua jema au ovu. Matumizi ya uwezo huu yamemsababishia mwanadamu mateso makubwa, na Mungu amejizuia ili kuheshimu uhuru wa mwanadamu wa kuchagua.

 

Shetani Mwovu

Shetani ni mwovu, na ili uovu upate kushamiri watu wema wanatakiwa kukaa kimya bila kufanya lo lote. Luther King aliwahi kusema, “Kufikia mwishoni mwa karne ya 20 wengi wetu hatutatubu kwa uovu mwingi tulioufanya, lakini ile hali inayotuzuia sisi kufanya cho chote”.

3. Yesu Aliteseka Na Aliteswa

Watu wake mwenyewe hawakumpokea, walimtukana, walikula njama dhidi yake, walimtesa na hatimaye wakamwua kwa mateso makali ya aina yake; baada ya kesi iliyoendeshwa kimizengwe mizengwe, ikiwa na mashahidi wa uongo, haikusikilizwa na jopo, hapakuwa na utetezi wala huruma. Soma (Zab 69:20) (Isa 50:6; 53:5) (Zek 13:6) (Mk 15:34) (Lk 22:44) (Ebr 2:10; 5:8; 13:12) (1Pet 1:11; 2:21; 3:18).

4. Paulo Aliteseka Na Aliteswa

Kama ilivyokuwa kwa wafuasi wa Yesu na watu wa Mungu wengi wa zama za kale
(Mdo 9:29; 13:50; 14:5,19; 16:22; 18:12; 21:36; 22:22; 23:10) (1Kor 4:12) (2Kor 4:9; 11:24) (2Tim 2:9; 3:11).

Hatutazamii Tofauti Yo Yote
Y
esu alisema, "Mtumwa hawi mkuu kuliko bwana wake. Ikiwa wamenitesa mimi, watawatesa na ninyi pia. Ulimwenguni humu mnayo dhiki. Lakini jipeni moyo! Mimi nimeushinda ulimwengu (Yn 15:20; 16:33). Paulo alisema, “Kila mtu anayetaka kuishi maisha ya kimungu katika Kristo Yesu atateswa” (2Tim 3:12). Katika vizazi vyote waamini wameteswa na kuuawa kwa kumfuata Kristo, hata huko Rwanda na Iran mwaka 1997. Hata leo yapo majaribu ambayo waamini wanapaswa kuyastahimili kwa ajili ya Kristo.

Kuteswa, Mdo 9:16.

Maudhi Na Chuki, Mt 5:11; 10:22.

Kupoteza Nafsi, Mt 10:39.

Kupoteza Mali, Jamaa, Mt 19:29.

Kupoteza Hadhi 1Kor 4:10; 2Kor 4:5.

Mauti, 2Kor 4:11; 12:10; Flp 1:29.

 

Je, Tunamtii Mungu Au Mwanadamu?

Jibu kutoka kwa kanisa linaloteseka, kwanza kabisa ni kulitii neno la Mungu. Na ikibidi tukubali adhabu inayoweza kutolewa na mwanadamu kwa ajili ya kumtii Mungu (Mdo 5:29; 4:19).

5. Jinsi Ya Kushinda Mateso

Shukuru katika mazingira yote.

Msifu Mungu katika mazingira yote (1Pet 4:12-19).

Omba kila wakati, kata rufaa mbinguni ili upate haki yako kutoka kwenye mahakama iliyo kuu kuliko zote.

Wasamehe, kwa kuwa hawajui watendalo.

Pigana vita vya kiroho, kwa kuwa mapambano yetu si dhidi ya nyama na damu (Efe 6:12).

 

Pengine Mungu anaweza akaamua kutuma tetemeko la ardhi kama alivyofanya kule Filipi ili kuwatoa gerezani Paulo na Sila; au akatuma malaika kama alivyofanya kwa Petro na kumtoa gerezani; au akaamua kutembea na wewe motoni (Mdo 16:25-30; 12:1-12) (Dan 3:24,25).

 

Ushauri Kutoka Kwenye Biblia

Tunapaswa kuwapenda adui zetu

Tunapaswa kuwabariki wale wanaotulaani.

Tunapaswa kuwatendea mema wale wanaotuchukia.

Tunapaswa kuwaombea wale wanaotutesa.

Usilipize ubaya kwa ubaya.

Wahudumie wanaoteseka.

 

(Mt 5:43-48) (Kut 23:4, 5) (Ayu 31:29) (Mit 24:17; 25:21, 22; 20:22; 24:29) (Mt 5:39-44) (Rum 12:14-21) ( Lk 6:27,35; 23:34) (1The 5:15) (Mdo 7:60) (Law 19:18) (1Pet 3:9) (1Pet 5:9-11).

Kwa Kumalizia Omba Kwa Ajili Ya Watu Ambao Hawajafikiwa Na Injili Hapa Ulimwenguni, Ukiwataja Kwa Majina

Iran

Jina la watu

Lugha yao

Idadi yao

Gilaki

Gilaki

2,400,000

Gurani (Bajalani)

Bajelan

20,000

Gurani (Bajalani)

Hawrami

18,000

Harzani

Harzani

24,000

Hazara (Khawari)

Hazaragi

604,000

 






 1985 - 2007

With many thanks to Pastor Dastan Mboera, Dar es Salaaam, Tanzania
and EAPTC Nairobi, Kenya for this revision and translation from the original English.
mboeradsk @ yahoo.com


© Dr Les Norman  The DCI Trust, UK
Permission is granted to provide copies at cost price for study purposes
but not for sale or commercial purposes. Freely you have received, so please freely give.

Support Pages   Index to All Lessons   School of Finances  

World Christian News   
Who Are We?   Site Index

www.dci.org.uk