1985 - 2007

 

38. Mrejeshe Mfalme

Support Pages   Index to All Lessons   School of Finances  
World Christian News   
Who Are We?   Site Index
 

Katika Biblia Yako Soma
Yeremia 8:20; Mathayo 13.

Mstari wa Kukariri
 “…Ufalme wa dunia umekwisha kuwa ufalme wa Bwana wetu na wa Kristo wake, naye atamiliki hata milele na milele” (Ufu 11:15).

Baadaye Zungumzieni Jambo Hili
Ni ishara gani za nyakati unazoweza kuziona hapa duniani? Ni matukio gani unayoyaona kwenye magazeti na kwenye TV ambayo yametabiriwa kwenye Biblia?

Jambo La Kufanya Kabla Hatujakutana Tena
Je, umebarikiwa na mafunzo haya? Kama umebarikiwa basi omba nafasi makanisani na kuwafundisha watu kile ulichokipata. Wakaribishe katika vipindi utakavyoandaa au waelekeze jinsi ya kuanzisha vikundi vyao.

Kazi Ya Kuandika Ya Stashahada
Chunguza andiko hili, 2Pet 3:10-17, na kisha andaa orodha ya majibu kumi kwa swali lifuatalo kwa kuzingatia kwamba Bwana anakaribia kurudi. “Sisi tunapaswa kuwa watu wa aina gani?

Tafakari Mstari Huu Neno Kwa Neno
Ufunuo 22: 20.

Tumia Dakika Moja Kuubadilisha Ulimwengu

Ombea taifa la Kongo (DRC). Idadi ya watu: 42,000,000 katika makabila 450.

Asilimia 21% ni madhehebu ya Kiinjili; asilimia 42% ni Wakatoliki

 

Wakati huu Mfalme wetu Yesu hayupo pamoja nasi, yupo mbinguni na anasubiri wakati wa Mungu ufike ili arejee kuja kuutawala ulimwengu kwa haki. Kila mmoja anataka kujua ni lini. Katika Mdo 1:7 Yesu alisema, “…Si kazi yenu kujua nyakati wala majira…”, lakini ametupa viashiria vingi vinavyotufanya tuelewe majira ambayo Bwana anatazamiwa kurejea.

1. Kuna Ishara Duniani

Awali ya yote, nabii zote zinazomhusu Mfalme ni lazima zitimilizwe. Yesu alituambia habari za matukio ya ulimwengu yatakayopelekea kurudi kwake, na kwa kadiri siku za mwisho zinavyozidi kupungua ni lazima tutazamie kuona ishara hizo kwa kiwango kikubwa (Mt 24:3-51) (Mk 13:1-37) (Lk 21:5-36).

Taifa Litainuka Juu Ya Taifa Jingine
Neno taifa ni ethnos lenye maana ya kundi la watu. Na ingawaje vita vya ulimwengu vimemalizika, lakini vita baina ya vikundi vya kikabila vinaendelea katika maeneo mbalimbali ya dunia kwa mfano Bosnia, Chechenya, Afghanistan, na Rwanda.

Maafa Yataongezeka
Kuongezeka kwa njaa, magonjwa, matetemeko ya ardhi na vimbunga ni ishara za ule mwisho.

Matukio Ya Kutisha Na Ishara Kuu
Madhara hayatakosa kuja, pengine yatasababishwa na uchafuzi wa mazingira unaotokana na milipuko, uharibifu wa misitu, ajali za nyuklia, au tofauti kubwa iliyopo kati ya maskini na matajiri. Baadhi ya manabii wanadhani kwamba matajiri wa Magharibi wanakaribia mwisho wa miaka ya ng’ombe wanono wa Yusufu (Mwa 41:17-40) na kwamba miaka ya ng’ombe waliokonda imekaribia. Wale ng’ombe waliokonda waliwameza wale walionona na hili linawakilisha hazina za kitaifa, lakini walikuwa wamekonda. Na kama ilivyokuwa wakati wa Yusufu, watu wanaweza kujikuta kwenye utumwa wa madeni bila fedha, bidhaa za kununua na kuuza, au ardhi, na ni lazima aje Mwokozi kama Yusufu.

Matukio Makuu Ya Kiroho
Yapo matukio ya kweli ya uamsho yanayoendelea kadiri Roho wa Mungu anavyotembea katika juhudi za kuleta mavuno kwa ajili ya Yesu. Yapo pia matukio ya uamsho usiokuwa wa kweli yanayoendeshwa na mapepo wachafu katika juhudi za kuvuruga kazi ya Mungu.

Israeli Ni Ishara Dhahiri Hapa Duniani
Baada ya miaka 1,900 ya kutawanyika duniani bila makazi, watu wa Mungu, Wayahudi, ambao pia hawakupendwa, wamerudi kwenye nchi yao kama ilivyotabiriwa (Amo 9:8-15).

Mihuri, Tarumbeta, Magojwa Na Bakuli
Saba kwa kila moja ya haya yanapatikana katika Ufunuo mlango wa 6 hadi wa 16, ambako tunaelezwa kuhusu matukio ya ghafla na ya ajabu hapa duniani. Lakini usijali, tazama juu! Hayo yote yanaashiria kurudi kwa Yesu ambako kutakuwa utatuzi wa masuala mengi, na jibu la maombi ya mamilioni wa watu ulimwengu mzima (Lk 21:25,26).

2. Kuna Ishara Katika Ufalme

Ufalme ni pale Mfalme anapotawala. Tunamwomba Mungu, “Ufalme wako uje”, na vitendawili vya Ufalme kwa mfano Mathayo 13 inatuonesha namna mambo haya yanavyotokea. Kutoka kwa marafiki wachache waliokuwa katika eneo la Msalaba, leo mamilioni ya watu kwa uaminifu na kwa furaha wamemfanya Yesu kuwa Mfalme wao.

Mfalme Anakuja

Kanisa Linajengwa
Yesu aliahidi kwa upendo mkuu akisema, “Nitalijenga kanisa langu” (Mt 16:18) (Efe 5:27), na ndicho kitu hasa anachokifanya siku hizi. Zaidi ya asilimia 50% ya watu waliowahi kuokoka, wameokolewa tangu mwaka 1900 na wengi wa hao ni kuanzia mwaka 1950. Watu 70,000 humpa Yesu maisha yao kila siku duniani kote. Mikutano mikubwa ya injili imewaleta kwa Yesu mamilioni ya watu kutoka Amerika Kusini, Afrika kusini mwa jangwa la Sahara, na sehemu za Russia, Uchina na Korea ya Kusini.

Inafanyika Toba Ya Kitaifa
Watu wanapotubu kwa ajili ya dhambi za taifa lao wanahimiza kurudi kwa Mfalme. Kwanini? Katika Mdo 3:13 Petro anawatuhumu watu wake kwa kumwua Yesu. Lakini kwa ukweli sio wao hasa waliotenda jambo hilo, bali viongozi wao. Petro akasema kwamba kama tutajihusisha na dhambi za mataifa yetu, na kutubu kwa niaba yao, na kumgeukia Mungu kwa niaba yao, Mungu atafanya yafuatayo (Mdo 3:19,20):

Utekelezaji wa Agizo Kuu Unasonga Mbele
Katika Mt 24:14 Yesu anasema kwamba ule mwisho hautakuja hadi injili hii itakapokuwa imehubiriwa katika mataifa yote. Neno mataifa hapa, ethnos, halina maana ya mataifa ya kisiasa mathalani India, lakini makundi ya kikabila, ambayo watu wake wameunganishwa na lugha moja na utamaduni mmoja. Miaka 200 iliyopita makumi ya maelfu ya mataifa yalikuwa hayajafikiwa kabisa; hata kufikia mwaka 1900, idadi ilikuwa bado ni ndogo. Leo hii wasomi wa masuala ya Umisheni wanajua idadi ya mataifa yaliyobakia ni kama 7,000 tu. Wanayajua mataifa hayo kwa majina na mahali yalipo. Mipango ipo na maombi yanafanyika ili kuwafikia wote.

3. Kwahiyo Sisi Tunapaswa Kuwa Watu Wa Namna Gani?

Katika 2Pet 3:10 -18 tunaambiwa kwamba kwa kuzingatia ujio wa siku ya Bwana, tunapaswa kuwa watakatifu, bila doa, bila lawama, tukihimiza kurudi kwake, tukikesha, tukisimama imara bila kuchukuliwa na mafundisho potofu, tukikua katika neema na katika kumjua Yesu.

Je, Tunaharakishaje Ujio Wa Siku Hiyo?
Kwa kuomba na kuutumikia Ufalme kwa njia ya kulijenga Kanisa, tukiziungama dhambi za taifa letu, na kukamilisha utekelezaji wa Agizo Kuu.

Kwa Kumalizia Omba Kwa Ajili Ya Watu Ambao Bado Hawajafikiwa Na Injili, Ukiwataja Kwa Majina

Iraq

Jina la watu

Lugha yao

Idadi yao

Anatolian Turk

Turkish

22,000

Bajelan (Shabak, Gura)

Bajelan

20,000

Circassian (Cherkess)

Adyghe

10,000

Dom Gypsy

Domari

50,000

Hawrami (Gurani)

Hawrami

22,000

 






 1985 - 2007

With many thanks to Pastor Dastan Mboera, Dar es Salaaam, Tanzania
and EAPTC Nairobi, Kenya for this revision and translation from the original English.
mboeradsk @ yahoo.com


© Dr Les Norman  The DCI Trust, UK
Permission is granted to provide copies at cost price for study purposes
but not for sale or commercial purposes. Freely you have received, so please freely give.

Support Pages   Index to All Lessons   School of Finances  

World Christian News   
Who Are We?   Site Index

www.dci.org.uk