1985 - 2007

 

40. Kwanini Watu Maskini Wawe Maskini Kiasi Hicho?

Nelson Mandela aliuelewa ubaguzi wa rangi na umaskini

Support Pages   Index to All Lessons   School of Finances  
World Christian News   
Who Are We?   Site Index
 

Katika Biblia Yako Soma
Luka 6

Mstari wa Kukariri
"Fumbua kinywa chako kwa ajili yake aliye bubu; uwatetee watu wote walioachwa peke yao; fumbua kinywa chako, uhukumu kwa haki; uwapatie maskini na wahitaji haki yao” (Mit 31:8,9).

Baaadaye Zungumzieni Jambo Hili
Ni kwa jinsi gani unavyoweza kuwa mikono ya Yesu, miguu yake na moyo wake kwenye mji unamoishi?

Jambo La Kufanya Kabla Hatujakutana Tena
Kama kikundi mwendeeni wakala anayefanya kazi miongoni mwa watu maskini na mjitolee kufanya kazi kwa ajili yao. Msijali kama wakala huyo ni Mkristo au la.

Kazi Ya Kuandika Ya Stashahada
Andika maelezo ya ukurasa mmoja ukiainisha jambo unalodhani limewapata watu na kuwafanya maskini.

Tafakari Mstari Huu Neno Kwa Neno
Y
eremia 22:16

Tumia Dakika Moja Kuubadilisha Ulimwengu

Ombea taifa la Bangladesh. Idadi ya watu ni 132,000,000. Ni maskini sana.

Asilimia 87% ni Waislamu; asilimia 10% ni Wahindu; na asilimia 0.08% ni wafuasi wa madhehebu ya Kianjili.

Watu ni wengi kupita kiasi, na nchi inakumbwa na mafuriko.

 

Siku moja Yesu alipokuwa akizungumza na umati wa watu ambao wengi wao walikuwa wanavijiji walioishi chini ya utawala wa kimabavu wa Warumi na viongozi wa kidini matajiri, aliwaambia, “Heri yenu ninyi mlio maskini, …” (Lk 6:17-20). Mara nyingi sisi tunapenda kufasiri maneno Yesu anayozungumza kuhusu maskini kumaanisha ni umaskiniwa kiroho, lakini neno Yesu analotumia hapa ni ptochos, lenye maana ya maskini anayetetemeka.

Biblia inataja maskini zaidi ya mara 245 na hii inaonesha jinsi Mungu alivyo na mengi ya kusema kuhusu umaskini. Suala hili lipo karibu na moyo wake na kamwe hautaji umaskani kama baraka, wala utukufu, au jambo la kufurahiwa, kinyume chake Biblia inasema ni laana.

1. Kwanini Watu Maskini Ni Maskini?

Baadhi ya watu ni maskini lakini si kosa lao; lakini ni kutokana na kunyonywa na kukandamizwa na watu wengine, dhambi za watu matajiri, viongozi wala rushwa, au mataifa yanayovamia na kutawala. Maneno ya Kiebrania ni rush na ani.

Maskini Wanyenyekevu Wa Bwana
Baadhi ya watu wa Mungu waliodhilika kwa umaskini na kukandamizwa wanaitwa maskini wanyenyekevu wa Bwana, na wanamlilia Bwana wao na kumtegemea yeye kwa unyenyekevu (Kut 1:11,12). (Neno ani ni la Kiebrania, na ptochos ni la Kigiriki).

Waathirika Wa Maafa
Watu wanaweza kuwa maskini pia kutokana na maafa yanayosababishwa na matukio ya asili, ajali, uchumi mbaya kitaifa, au wamezaliwa wakiwa vilema, na kwa kweli hawana kosa katika yote hayo. Wanaweza wakawa ni watu wadogo, au wasio na ulinzi wala msaada wo wote kama vile wajane na yatima. (Maneno ya Kiebrania ni ebyon, dallah, na dal).

Dhambi Ya Mtu Binafsi
Watu wengine wengi ni maskini kutokana na dhambi zao wenyewe na hilo ni kosa lao wenyewe (Ayu 33:3) (Mit 13:25; 24:30; 21:5; 22:16; 21:17; 28:22) (Kum 28:48)(Neno la Kiebrania ni chaser). Dhambi binafsi inasababisha umaskini, lakini machungu ya umaskini huo yanasababisha dhambi nyingine binafsi kama vile wizi na ulevi unaosababisha uovu, magonjwa, na vurugu (Mit 30:9; 30:7).

2. Kwa Namna Gani Wanaweza Kubarikiwa?

Yesu anawaita maskini heri kwa sababu anajua wamebarikiwa na Mungu, Mungu wa haki yote, Mungu anayerekebisha mambo yote kuwa sawa. Watu wengi walio maskini hawajawahi hata kusikia habari hizi, licha ya kufungua mioyo yao na maisha yao ili kupokea hiyo baraka.

Ni Nini Jibu La Mungu?
Katika Mithali 31:9 waamini wanaelekezwa jambo la kufanya. “Fumbua kinywa chako, uhukumu kwa haki; uwapatie maskini na wahitaji haki yao”. Hatima ya watu maskini ipo mikononi mwetu, ingawa zoezi hili linaweza likawa hatari kwetu kama lilivyokuwa kwa watu waliowatetea maskini kama vile Amy Carmichael, William Wilberforce na William Booth.

Mungu Anawaona Watu Maskini Kuwa Wa Thamani
Soma kutoka Ayubu 36:15, Zaburi 34:6; 35:10; 113:7, 8; ili upate kujua kwamba habari njema za Mungu kwa maskini ebyon, dal na dallah ni Yesu mwenyewe (Lk 7:22).

Sisi Ni Mikono Ya Yesu
Wengine wananukuu 1Yoh 3:17 au Yak 2:15; 1:27 na kusema kwamba tunapaswa kuwasaidia ndugu zetu kwanza. Ni sawa kwa sababu wapo wengi sana wanaopambana katika udhaifu wao, lakini hata hivyo maskini, chaser, ambaye pengine hapendwi au pengine hana shukrani, ana huruma na neema kwa Mungu. Mungu anasema nao kipekee katika Zab 23:1, Zab 34:9,10. Soma pia Ayu 29:15,16.

3. Maskini Wanabarikiwaje Basi?

Yesu aliposema, “Mmebarikiwa ninyi mlio maskini,...” alikuwa akiwatazama wafuasi wake (Lk 6:20). Hao ni maskini ambao pia ni wafuasi wa Yesu ndio wanaobarikiwa kupitia imani yao kwa Mungu.

Kubarikiwa Na Mungu Anayejali

Mungu anaelewa machungu ya umaskini kuliko mtu mwingine ye    yote, kwa sababu pale msalabani Mungu mwenyewe kama Yesu alipata mateso ya kusalitiwa, kunyimwa haki, kukandamizwa na kukosa vitu vyote.

§         Ayubu anawatetea maskini, (Ayu 1:16).

§         Zaburi za Daudi zinawapa maskini tumaini.

§         Isaya anatabiri msaada kwa watu wanaowapenda maskini, (Isa 58:6-12).

§         Hosea anatujulisha jinsi Mungu anavyofanya watu wampende, (Hos 11:4).

§         Yeremia anauliza kama kweli unamfahamu Bwana, (Yer 22:16).

§         Yesu alipakwa mafuta na Mungu ili awahudumie akina ptochos, ambao ni wanyenyekevu wa Mungu walio maskini (Lk 4:18,19).

§         Paulo anaweka fundisho katika matendo, (Gal 2:10; 6:10) (2Kor 8:13).

§         Yakobo analipa kanisa changamoto, (Yak 2:5, 14-16).

§         Kanisa la Petro lilijali, (Mdo 4:34,35).

§         Neno la mwisho la Yohana, (1Yoh 3:17,18).       

Kubarikiwa Kwa Kupokea Msamaha
Katika Yesu kuna msamaha wa Mungu kwa dhambi zote binafsi zinazosababisha umaskini. Safari ya kwenda Jehanum iliyo halisi inaweza kusitishwa na mwelekeo wake kugeuzwa kabisa.

Kubarikiwa Kwa Neema Ya Mungu
Y
esu anawapa watu maskini uwezo dhidi ya majaribu. Mikono iliyotumika katika wizi sasa inamtumikia Mungu, familia na watu wengine (Efe 4:28).

Kubarikiwa Na Watu Wa Mungu
Mungu anaamuru waamini wenye mali na uhuru kuwafadhili watu maskini na kusimama kinyume na vitendo vyote vya uonevu vinavyowashikilia mamilioni ya watu kwenye umaskini wa rush. Katika Mt 25:35 Yesu anaelekeza la kufanya.

Katika mazingira hayahaya ya umaskini, wafuasi wanaagizwa kuwapenda adui zao, ambao wanaweza kuwa ndio haohao maskini wanaokuibia, na sio kuwapenda wale tu wanaowapenda ninyi. Tunapaswa kufanya wema wetu si kwa wale wanaotufanyia wema tu, tusiwahukumu, na tusiwakopeshe wale tu watakaoturudishia. Utakapowapa maskini, na wewe utapewa (Lk 6:27-38). Hawataweza kukulipa lakini Mungu atakulipa (Mit 19:17).

Injili inawabariki maskini wanaomkimbilia Kristo, na Injili hiyohiyo inawabariki matajiri wanaomkimbilia Kristo. Lakini kama tajiri atakuwa ni sababu ya watu wengine kuteseka kwa umaskini, Yakobo anatoa tahadhari (Yak 5:1-6).

 

Kwa Kumalizia Omba kwa Ajili Ya Watu Wa Ulimwengu Ambao Hawajafikiwa Na Injili, Ukiwataja Kwa Majina

                                     

Japan

Jina la watu

Lugha yao

Idadi yao

Amami-Oshima

Amami-Oshima

16,000

 





 1985 - 2007

With many thanks to Pastor Dastan Mboera, Dar es Salaaam, Tanzania
and EAPTC Nairobi, Kenya for this revision and translation from the original English.
mboeradsk @ yahoo.com


© Dr Les Norman  The DCI Trust, UK
Permission is granted to provide copies at cost price for study purposes
but not for sale or commercial purposes. Freely you have received, so please freely give.

Support Pages   Index to All Lessons   School of Finances  

World Christian News   
Who Are We?   Site Index

www.dci.org.uk