1985 - 2007

 

44. Yesu Aliishije?

Fundi seremala anaweza kuubadili ulimwengu!

Support Pages   Index to All Lessons   School of Finances  
World Christian News   
Who Are We?   Site Index
 

Katika Biblia Yako Soma
Wafilipi 4:2-20

Mstari wa Kukariri
Na Mungu wangu atawajazeni kila mnachokihitaji kwa kadiri ya utajiri wake, katika utukufu, ndani ya Kristo Yesu (Flp 4:19).

Baadaye Zungumzieni Jambo Hili
Zungumzieni kuhusu kanuni mlizoziona katika maisha ya Yesu na Paulo. Je, wewe huwezi kuishi kama wao?

Jambo La Kufanya Kabla Hatujakutana Tena
Andaa bajeti ya familia yako ya kila mwezi ukionesha mapato na matumizi. Weka orodha ya mapato yanayotarajiwa upande mmoja na matumizi yanayotarajiwa upande mwingine. Je, pande mbili zinalingana? Mapato yakizidi matumizi ni baraka, kinyume chake ni matatizo!

Kazi Ya Kuandika Ya Stashahada
Soma Kumbukumbu La Torati mlango wa 28 na kisha orodhesha yote yaliyosemwa kuhusu mafanikio na umaskini. Andika kwenye ukurasa mmoja ukionesha kila mojawapo linavyokuja.

Tafakari Mstari Huu Neno Kwa Neno
Kum 28:47

Tumia Muda Mfupi Kuubadilisha Ulimwengu

Ombea taifa la Djibouti. Idadi ya ni 473,000. Huko kuna Waislamu Wasomali na Waarabu. Wakristo ni wachache katika taifa hilo lililoko katika pembe ya Afrika. Ni jangwa na joto.

 

Mungu Alikuwa Na Mtoto Mmoja, Naye Alikuwa Mmishenari

Yesu aliishije? Kwa namna gani aliweza kujinunulia chakula na kulipa bili zake nyingine? Je, alibadili mawe kuwa mkate, na uwezo alikuwa nao, au alihudumu kama mtu mwenye uwezo wa Roho Mtakatifu? Maandiko yanatuonesha kwamba hilo la pili ndilo sahihi (Flp 2:6-8) (Mdo 1:2).

Hatujui majibu yote, lakini Biblia inatoa nuru ingawa haioneshi waziwazi ni njia ipi mojawapo iliyotumika. Hebu kwanza tushughulikie swali moja muhimu.

Je, Yesu Alikuwa Mtu Maskini?

Watu wengi na wachungaji watajibu, “Ndiyo”. Watu wanaonekana kuwa na mawazo kwamba kuna namna ya utakatifu au unyenyekevu katika umaskini, ingawa Biblia inasema ni laana (Kum 28:47).

Ya Nini Mtu Maskini Kuwa Na Mweka Hazina?

Je, katika maskini unaowafahamu kuna mmojawapo aliye na mweka hazina wa kuangalia mahesabu ya fedha zinazoingia na kutoka? Jambo moja ni wazi, kwamba Yesu alikuwa na namna ya kupata fedha kwa ajili yake, kwa ajili ya watu 12, na kwa ajili ya kutoa sadaka. Maskini hawezi kuwa na mweka hazina, lakini Yesu alikuwa naye. Kwahiyo kulikuwa na fedha; lakini zilitoka wapi?

Yesu Alichagua Udhaifu

Siku hizi kila mmoja anatafuta kuwa na nguvu lakini Yesu alichagua kwa dhaifu, na wepesi wa kushambuliwa na kudhurika; na kumtegemea Baba yake na rafiki zake.

  1. Alichagua kuzaliwa katika hali ya kimaskini.
  2. Aliamua kuishi kwenye familia ya mfanyakazi wa kawaida.
  3. Alichagua kuwa mfanyakazi wa kawaida katika jamii ya kawaida. Alijiweka kwenye mazingira ya kuweza kuathiriwa na hali ya uchumi wa mahali alipokuwa anaishi, na kuwategemea wengine pia.
  4. Alikuwa na upako wa furaha lakini pia alijua mateso ya watu waliomzunguka (Isa 53:3).
  5. Yesu aliamua kukaa bila vitu ambavyo watu husema ni muhimu. Alisema hana mahali pa kukilaza kichwa chake, pengine hapa akiwa na maana ya mali alizokuwa nazo, kwa sababu kila mara alikaribishwa kwenye nyumba nzuri. Kwahiyo alifanya matumizi na madeni kuwa ya chini kabisa. Tunajua alichagua kulala nje kwa siku 40.
  6. Alifanya kazi ya kuunda na kutengeneza samani mpaka alipofikia umri wa miaka 30.
  7. Alikubali malazi na ukarimu. Tunamwona Yesu nyumbani kwa Zakayo, nyumbani kwa Mathayo, kwa Simoni yule Farisayo, kwa Martha na Mariamu wa Bethania, kwa mamamkwe wa Petro; na kwingineko.
  8. Alikubali pia kutegemezwa na wanawake (Lk 8:3).
  9. Aliwaruhusu wafuasi wake kuvunja sheria za kanisa ili kujipatia riziki kutoka kwa Mungu (Mt 12:1-8).
  10. Wafuasi wake walienda mjini kufanya manunuzi (Yn 4:8), pia walivua kwa ajili ya kula na kuuza.
  11. Palikuwa na miujiza ya upatikanaji wa riziki lakini hii ilikuwa ni mara chache, na utaratibu huo haukuwa desturi. Mifano: kupatikana kwa sarafu kwenye kinywa cha samaki; chakula cha kijana mdogo kushibisha watu 5000; na mwujiza wa kuvuliwa samaki wengi chakula cha ufufuko.

Ni Wa Kawaida Tu!

Kitu Mungu anachotaka kutuonesha kupitia kwa habari za Yesu ni kwamba kuna upatikanaji wa riziki kwa njia za miujiza wakati tunapohitaji, lakini kwa kawaida riziki kwa watendakazi wa saa ya kumi-na-moja hutoka kwa Mungu na kuwajia kwa matukio ya kawaida ya kila siku na kwa kupitia kwa watu wa kawaida ambao Mungu anawaleta kwako. Kaza mwendo kuenenda katika utakatifu, katika upole na kwa kuishi kwa ajili ya wengine, nawe utaona jinsi Mungu atakavyojenga daraja imara chini ya miguu yako unapotembea juu ya mwujiza wa imani kwake na kwa neno lake (Yn 6:35).

Paulo Aliishije?
Na sasa, vipi kuhusu Paulo, mtu aliyepeleka injili Ulaya, na kuandika nyaraka zilizo nyingi katika Agano Jipya.

Ni Nani Aliyemtegemeza Paulo Katika Huduma Yake?
Hakutegemezwa na kanisa la Antiokia kwa sababu isingewezekana katika siku hizo. Katika matukio yote Paulo alipelekwa na Roho. Makanisa yalimtegemeza, lakini pia makanisa yalisitisha misaada yao. Mara moja tu kanisa moja lilimtegemeza (Flp 4:16).

  1. Msaada kutoka Antiokia ungeweza kupatikana mara kwa mara; lakini wangewezaje kujua mahali alipokuwa Paulo? Wakati huo hapakuwepo na njia za kisasa za kufanya malipo kama vile kadi, mabenki, rejista, na simu.
  2. Kama ilivyokuwa kwa Yesu, Paulo pia alikubali kufanyiwa ukarimu hata kutoka kwa wakimbizi kama Prisila na mumewe Akila katika nyumba ya hali ya chini (Mdo 18:3).
  3. Na kule Kuprosi, familia ya Barnaba ilikuwa na nyumba; kwahiyo walikaa nao!
  4. Mle gerezani watu walileta chakula na baadaye yule askari magereza aliwaandalia chakula (Mdo 16:34).
  5. Kule Filipi alikaa kwa Lidia, yule mwanamke mfanyabiashara aliyekuwa ameokoka karibuni (Mdo 16:15).
  6. Paulo alikuwa na eneo lake la kufanyia kazi, alitengeneza na kuuza bidhaa sokoni; akajipatia riziki yake na ya watu wengine (Mdo 18:3; 11:26; 20:24) (2The 3:8).
  7. Na Walawi, ambao ni kama watendakazi wa Kikristo wa Agano la Kale, walikuwa wakitegemea Hekalu. Lakini hata Hekalu liliposhindwa kuwategemeza walikuwa na shamba lao wenyewe; walilima mazao na kuuza (Hes 3) (Hes 18:21; 35:2,6,7) (Neh 13:10).

Theolojia Ya Paulo Ya Kuishi

Paulo, mwanatheolojia mkuu wa wakati wake alielezea namna ya kuishi kwa kusema, “Lakini kwa neema ya Mungu nimekuwa hivi nilivyo; na neema yake iliyo kwangu ilikuwa si bure, bali nalizidi sana kufanya kazi kupita wao wote; wala si mimi, bali ni neema ya Mungu pamoja nami” (1Kor 15:10).

Umeshaona ya kwamba huhitaji kuwa mtu mwenye imani kubwa ili uweze kuitikia wito wa Mungu. Watu wakuu sana katika Agano Jipya wametuonesha jinsi lilivyo jambo la moja kwa moja kuishi katika neema na riziki za Mungu.

 

Kwa Kumalizia Omba Kwa Ajili Ya Watu Wa Ulimwengu Ambao Hawajafikiwa Na Injili, Ukiwataja Kwa Majina

 

Libya

Jina la watu

Lugha yao

Idadi yao

Zuara (Zwara, Zuraa)

Zuara

33,000




 1985 - 2007

With many thanks to Pastor Dastan Mboera, Dar es Salaaam, Tanzania
and EAPTC Nairobi, Kenya for this revision and translation from the original English.
mboeradsk @ yahoo.com


© Dr Les Norman  The DCI Trust, UK
Permission is granted to provide copies at cost price for study purposes
but not for sale or commercial purposes. Freely you have received, so please freely give.

Support Pages   Index to All Lessons   School of Finances  

World Christian News   
Who Are We?   Site Index

www.dci.org.uk