1985 - 2007

 

54. Ustahimilivu

Bi. Cory Aquino alistahimili hata kuwaletea Wafilipino mapinduzi ya amani

Support Pages   Index to All Lessons   School of Finances  
World Christian News   
Who Are We?   Site Index
 

Katika Biblia Yako Soma
Danieli 10

 

Mstari Wa Kukariri
Basi mtiini Mungu. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia (Yak 4:7).

 

Baadaye Zungumzieni Jambo Hili
Katika Mdo 16:6-10 Roho Mtakatifu alimzuia Paulo, katika 1The 2:18
Shetani alimzuia, na katika 1Kor 16:12 Apolo mwenyewe alikuwa hataki. Unasemaje kwa nafsi yako; ni nani anayekuzuia?

 

Jambo La Kufanya Kabla Hatujakutana Tena
Kila mmoja wenu atafute waamini wawili wapya kutoka kwenye kanisa lo lote. Watembelee na kuwatia moyo. Huenda ikawa wanakabiliwa na upinzani wa kila namna.

 

Kazi Ya Kuandika Ya Stashahada
Shetani alimzuia askari mzoefu kama Paulo. Wewe unafikiri alimudu vipi kumzuia? Andika maelezo ya ukurasa mmoja.

 

Tafakari Mistari Hii Neno Kwa Neno
1Pet 5:6-11

 

Tumia Muda Mfupi Kuubadilisha Ulimwengu

Ombea taifa la Yordani. Idadi ya watu ni 4,000,000; ni Waarabu. Asilimia 94% ni Waislamu; na watu 7,000 ni wafuasi wa madhehebu ya Kiinjili.

 

 

Je, umewahi kuona ni nini kinachotokea mtu anapoamua kumfuata Yesu? Wanafamilia ghafla wanakuwa wataalamu wa mambo ya kidini, na malumbano yanaendelea. Ukitaka kuona jinsi tabasamu linavyotoweka haraka katika nyuso za watu, taja mambo kama ubatizo wa maji, kujazwa Roho Mtakatifu na kunena kwa lugha.

 

1. Mtu Anachukia!

Katika Efe 6:12 tunaambiwa kwamba vita vyetu si dhidi ya nyama na damu; kwahiyo ni Shetani na mtandao wake mwovu ndiye anayepinga:

 

Wokovu Wetu

Ni pale Shetani anapolazimika kuachia, na mbaya zaidi kwake, ni pale Mungu anapoingia ndani mwako.

Ubatizo wa Maji

Ni pale utu wa kale wa dhambi unapokatiliwa mbali.

Ubatizo wa Roho

Ni pale utu mpya unapowezeshwa.

 

Shetani anaposhindwa, hatua inayofuata ni kujaribu kuwafanya wafuasi wapya wawe vipofu kwa maana ya kwenda kanisani kila Jumapili na kutoa senti kidogo kila wiki, basi.

 

2. Songa Mbele, Kwa Ajili Ya Yesu

Sasa ukithubutu kuombea umisheni, ni lazima uchukue tahadhari kwa milipuko ya hofu ndani yako, matatizo ya kifamilia, na hata kutokuelewana ndani ya kanisa. Hii ni kwa sababu umisheni ni kama gari la kumbebea mfuasi wa Yesu aliyezaliwa mara ya pili, anayeishi maisha ya ushindi, aliyejazwa Roho, anayeongozwa na Roho; ili kuleta mabadiliko makubwa katika ulimwengu unaomzunguka kwa ajili ya Kristo.

 

Biblia inatuambia kwamba watu wasiokuwa na maono huangamia (Mit 29:18), na hilo ndilo Shetani analolitaka. Kwanza anataka uangamie kwa kuchoshwa na maisha ya ukristo, na kisha anataka ulimwengu wa watu atakaoangamia nao milele. Maisha yako yakiwa mikononi mwa Roho Mtakatifu inaweza kuwa sababu ya watu wengi, wake kwa waume, kupokea uzima wa milele.

 

Ni Mmoja Tu Kati Ya Mia Moja

Inakuwaje kwamba ni mmoja tu kati ya waamini 100 wanaokubaliana na umisheni, ambao kweli wanashiriki shughuli za umisheni? Je, kuanza maisha ya ndoa, au ajira, au masomo, au ukata vyaweza kuwa sababu ya kweli? Au kuna mikono ya siri ambayo inakula njama kuwazuia waamini wapya, wachungaji, wazee, na hata kanisa kwa ujumla lisitekeleze Agizo Kuu?

 

3. Ni Nani Anayekuzuia Wewe?

 

Je, Ni Roho Mtakatifu?
La kushangaza ni kwamba ni Mungu; Roho Mtakatifu atakuwa wa kwanza kukuzuia wewe kama rafiki. Ikiwa uko tayari kutumika unafanyika mtu wa thamani kiasi kwamba Roho Mtakatifu atakuzuia iwapo ataona kwamba kuna kasoro katika mwelekeo wako, mbinu zako au hata muda wako (Mdo 16:6-10) (Isa 30:21).

 

Je, Ni Pepo Mchafu?
Kama kuna jambo wasilotaka kulisikia roho za mpinga-Kristo ni habari za kuhubiriwa Injili kwa mataifa yote na kurejea kwa Mfalme. Kutoka ndani ya ngome zao za imani mbalimbali za ulimwengu huu kama vile Uislamu, hutukebehi kwa kusema, “Hamwezi kuingia hapa. Angalia jinsi tulivyo jeshi kubwa; jinsi tulivyo wengi tunaopingana na ninyi wachache mliogawanyika!”. Lakini katika 1Nya 11:4,5 kwa msaada wa Mungu Yerusalemu ilianguka pamoja na ubishi wake; na hivi karibuni Ukuta wa Berlin ulianguka, na tumeshuhudia pia kuporomoka kwa Ukomunisti. Wakati mwingine tunaweza tukadhani kwamba sisi ni wadogo na wanyonge kama theluji, lakini chembechembe za theluji zinapokusanyika pamoja huuzuia mji!

 

Je, ni nini kimewatokea wale mapepo wakuu wa Uyunani na Uajemi, au miungu wa siku za Elia, na wenzi wao wa Kirumi na Kiyunani katika siku za Paulo, Ziasi na Herme kwa mfano? Je, unafikiri wamefutika? La hasha! Hawa ni viumbe wasioathiriwa na muda au kifo; na mkakati wao wa kudumu ni uovu na kuwashikilia kwenye giza watu wa vizazi vyote. Kwahiyo mkuu wa anga la Mexico akijua unakuja anaweza akaandaa migomo kwa ajili yako ili kukukatisha tamaa kabla hata hujaanza safari. Kwahiyo wala usishangae ukiona mgogoro wa ghafla unazuka kwenye familia au kwenye kikundi wakati hukuutazamia kabisa.

 

Je, Ni Roho Yako Mwenyewe?
Watu wengi ambao hawajafikiwa na Injili wako tofauti sana na sisi, na si watu wengi waliookoka ambao wako tayari kwenda kuishi nao na kuwaonesha Yesu. Tunaweza kuziona sababu zake katika Mwa 12:1-3, pale Abramu anapoitwa na Mungu. Shetani ni bingwa wa kutia mambo chumvi, na vilevile kutia watu hofu.

 

Vikwazo Vya Kijiografia

Ni kwa sababu tunalazimika kuiacha nchi yetu tuliyoizoea.

Vikwazo Vya Kitamaduni

Ni kwa sababu tunalazimika kuwaacha watu tuliowazoea na desturi zetu.

Changamoto Za Kijamii

Ni kwa sababu tunalazimika kuiacha familia na kanisa, na kuwaendea watu ambao tunawashuku na wao pia wana mashaka na sisi.

Hofu Binafsi

Mawazo hutunyima usingizi usiku tunapokuwa tukipambana na hofu ya kutokumudu mambo fulani fulani, hofu ya mabadiliko katika maisha, hofu ya kukosekana fedha au kushindwa katika lugha. Ukweli ni kwamba tumezoea starehe na urahisi wa mambo; tukienda kanisani tunakuta tumeshaandaliwa kila kitu. Tunapokwenda mahali pengine, yawezekana sisi tukawa ndio kanisa kwa ajili ya mtu mwingine!

 

4. Kulishinda Giza

Zishinde njama dhidi yako kwa kuchukua hatua za Kimungu:

Fuata wito wa Mungu; ukisukumwa na upendo wa Kristo (2Kor 5:14).

Ukubali kuwa mwanafunzi hadi ukomae. Ushindi hupatikana kutoka penye udhaifu kwa maombi, vita vya kiroho, hekima na kutegemezwa na ushirika wa viongozi na marafiki wanaotaka kuona mafanikio yako.

 

Uwe tayari kufundishwa Biblia na stadi.

Ukubali kujifunza kwa kufanya kazi.

Hatimaye, uwasaidie wengine walio wachanga.

 

 

Kwa Kumalizia Omba Kwa Ajili Ya Watu Wa Ulimwengu Huu Ambao Hawajafikiwa Na Injili, Ukiwataja Kwa Majina

 

Oman

Jina la watu

Lugha yao

Idadi yao

Mahra

Mahri

109,000

Persian (Irani)

Farsi, Western

38,000

Shihuh

Arabic, Shihhi Spoken

10,000




 1985 - 2007

With many thanks to Pastor Dastan Mboera, Dar es Salaaam, Tanzania
and EAPTC Nairobi, Kenya for this revision and translation from the original English.
mboeradsk @ yahoo.com


© Dr Les Norman  The DCI Trust, UK
Permission is granted to provide copies at cost price for study purposes
but not for sale or commercial purposes. Freely you have received, so please freely give.

Support Pages   Index to All Lessons   School of Finances  

World Christian News   
Who Are We?   Site Index

www.dci.org.uk