1985 - 2007

 

59. Majaribu

Rais Nixon wa Marekani aliitwa kusimama lakini akaanguka kwenye jaribu

Support Pages   Index to All Lessons   School of Finances  
World Christian News   
Who Are We?   Site Index
 

Katika Biblia Yako Soma
1Tim 6:3-21; Dan 4:28-37; 1Fal 19

Mstari wa Kukariri
Ushiriki taabu pamoja nami, kama askari mwema wa Kristo Yesu. Hakuna apigaye vita ajitiaye katika shughuli za dunia, ili ampendeze yeye aliyemwandika awe askari. Hata mtu akishindana katika machezo hapewi taji, asiposhindana kwa halali (2Tim 2:3-5).

Baadaye Fanyeni Haya
Gawanyikeni katika makundi mawili na kisha ulizaneni maswali yahusuyo uadilifu na uaminifu.

Jambo La Kufanya Kabla Hatujakutana Tena
Kama nyumbani kwako kuna vitu visivyostahili kuwapo, kwa mfano majarida, vitabu, video na sanamu; vilete na kwa pamoja mvichome moto kwa jina la Yesu.

Kazi Ya Kuandika Ya Stashahada
Andika taarifa ya ukurasa mmoja ukielezea jinsi majaribu yanavyoweza kukuathiri.

Tafakari Andiko Hili Neno Kwa Neno
2Tim 2:20,21

Tumia Muda Mfupi Kuubadilisha Ulimwengu

Ombea taifa la Uingereza. Idadi ya watu ni 46,000,000; wengi ni watu wa kawaida waliopotea kiroho. Wengi wanatazamia uamsho mwingine; makanisa mengi yamehuishwa.

 

Mpango wa Mungu sikuzote ni kuinua viongozi watakaomtumikia kwa uaminifu maisha yao yote; lakini mpango wa Shetani ni kumpiga mchungaji ili kwamba kondoo wa kundi lake watawanyike. Sisi hatukosi kuzijua fikira zake zinazoweza kutuletea hatari kama hizo (Zek 13:7) (2Kor 2:11).

Majaribu

Kule nyikani Shetani alimjaribu Yesu kwa kumshawishi atumie vibaya nafasi yake na uweza wake wa kiroho ili kujipatia riziki; kisha akamshawishi achukue njia ya mkato ili kuepuka mateso; na hatimaye Shetani akapendekeza kujikweza. KiIa wakati Yesu alisema, Hapana! Uamuzi utakaoufanya sasa unaweza kuokoa maisha yako baadaye.

Majaribu mengine yanayowakumba viongozi yanaitwa ‘wasichana, madaraka na dhahabu’.

Wasichana (Wavulana !), Matumizi Mabaya Ya Ngono

Ukiruhusu sikio lako kusikia maneno ya mapenzi au jicho lako kuona picha za mapenzi, kunaweza kukusukuma kufanya ngono nje ya ndoa, na hasa unapokuwa mpweke, unapokuwa kwenye mawazo mazito, au unapokuwa safarini. Anguko litaathiri huduma, ndoa na heshima yako; na wengi hawatakuamini tena (Mit 6:20-35; 5:7-14).

 

Madaraka, Matumizi Mabaya Ya Nafasi

Utaweza kusikia majivuno ya watu kama vile, ‘mimi’ ndiye niliyefanya hili na lile, badala ya kumtukuza Mungu. Kiburi kilisababisha anguko la Shetani na tangu hapo amedanganya viongozi wengi (Dan 4:28-37) (Mit 16:18; 29:23).

 

Dhahabu, Matumizi Mabaya Ya Fedha

Wivu na tamaa ya kuwa na nyumba kubwa, magari ya kifahari, saa za dhahabu, mavazi ya kifahari, na usafiri wa daraja la kwanza; yote hayo bila shaka yatamsababishia mtu madeni na kuathiri utoaji wa sadaka na kusababisha matatizo makubwa ya fedha (1Tim 6:6-10).

 

Lililo Bora Kuliko Yote- Usianguke!

Uwe mwangalifu na udanganyifu wa moyo wako mwenyewe (Yer 17:9)

Macho yako yasiondoke kwa Yesu (Ebr 12:2)

Nyenyekea mbele za Mungu, Shetani asije akakudhili (1Pet 5:5,6)

Mkaribie Mungu (Ayu 33:14)

Watu husema, “Ni kwa neema ya Mungu tu…”. Ipo neema kutoka kwa Mungu, kwahiyo hakikisha unaipokea hiyo (2Tim 2:1). Mtafute rafiki aliye mwaminifu, kisha mwongee. Mruhusu akuulize maswali saba yafuatayo:

Maswali Ya Uadilifu

  1. Je, katika kipindi cha wiki moja iliyopita umekuwa na mwanamke (au mwanamume) mahali katika mazingira yanayoonesha kwamba mlikuwa na maridhiano hatari na ya siri?
  2. Je, kuna wakati matumizi yako ya fedha yamekosa uadilifu?
  3. Je, umejihusisha na kitu cho chote kinachohusiana na ngono?
  4. Je, umetumia muda wa kutosha katika kusoma na maombi?
  5. Je, umetenga muda wa kutosha kwa ajili ya familia yako?
  6. Je, umetimiza matakwa ya wito wako?
  7. Je, umemdanganya Mungu, umenidanganya mimi au umejidanganya mwenyewe?

Baraka Au Fadhaa?

Baada ya Shetani, adui mkubwa wa kiongozi anayefuata, ni kiongozi mwenyewe. Mfano mzuri ni Eliya. Katika Wafalme wa Kwanza mlango wa 19 alizuia mvua isinyeshe na kusababisha matatizo ya kiuchumi kwa taifa; alimfufua mtoto; aliita moto kutoka mbinguni; aliua manabii wa uongo 400; aliruhusu mvua inyeshe, na kisha akakimbia sana. Mtu wa namna gani huyu! Lakini sasa Jezebeli anapomtishia, Eliya anaishiwa nguvu kabisa na kuchoka. Hawezi kukabiliana na cho chote wala kufanya tendo lo lote la kinabii. Hana nguvu hata za kumtafuta tena Mungu kwa ajili ya neno lake.

Eliya Alishakata Tamaa

Anamwacha mtumwa wake, analikimbia tatizo, anaishia mahali pakame na kumwomba Mungu autwae uhai wake. Musa naye aliomba maombi kama hayo (Hes 11:15), na hilo linaweza kumtokea mtu ye yote. Kiongozi anapojishughulisha na masuala ya kifamilia, matatizo ya kifedha, kanisa na mipango ya baadaye, mzigo unaweza kuwa mzito sana na kumsababishia uchovu mkubwa na hata kushindwa (1Fal 19:3-5).

 

Majibu Ya Mungu Yalikuwa Nini?

Mungu hakukemea, badala yake alionesha huruma; alimpa chakula kizuri, kinywaji na pumziko. Mungu anamwondolea Eliya kutokuamini na kujihurumia kwake na kisha anamwongoza kwenye tukio jingine jipya (1Fal 19:5-9). Baada ya ule upepo, tetemeko na moto, Mungu anamnong’oneza Eliya na kumwambia kazi haijaisha bado. Kisha anamrejesha kwa njia aliyoijia ili kuwapaka mafuta viongozi wapya wawili na kujipatia waamini wengine 7,000! Anamtii Bwana na huduma yake inasonga mbele kwa uweza (2Fal 1&2).

Kuushinda Uchovu

Spiringi ikiwa imevutwa sana inabidi iyeyushwe na kutengenezwa upya. Halikadhalika na sisi tunapofanya kazi kupita uwezo wetu. Kuushinda uchovu sasa kunahitaji miezi kadhaa ya kutengenezwa upya.

Namna Ya Kuulinda Moyo Na Nia

Fadhaa inahusika na mioyo ambayo hugandamizwa na nguvu moja zaidi, na akili huufanya mzigo kuwa mkubwa kupita kiasi, na zisiweze kufanya maamuzi mazuri.

Paulo katika Flp 4:2-9 anasema kwamba Mungu wa amani na amani ya Mungu itawalinda mioyo yenu na nia zenu wakati ~

Mnaposhughulikia mahusiano yenye matatizo kwa unyenyekevu na toba.

Mnapoendelea kufurahi katika Bwana, kama jambo la hiari kwenu.

Mnapokuwa wapole, bila maudhi, kwa kuwa Bwana yu karibu, na tumaini lipo.

Mnapokuwa hamjisumbui kwa neno lo lote, bali ni kumwambia Mungu na kushukuru.

Mnapoamua kutafakari juu ya mambo yaliyo ya kweli, na si yaliyo tishio.

Mnapoamua kutafakari kuhusu mambo yaliyo mema na ya kupendeza, na si ya kinyume na ya giza.

Kwa kila jaribu Mungu anaahidi njia ya kutokea (1Kor 10:13). Na hii inaweza kuhusisha hata mambo ya kiutendaji ya usimamizi wa muda, fedha na madeni; na kusema, Hapana kwa baadhi ya watu, miradi na taarifa za maandishi.

 

Kwa Kumalizia Omba Kwa Ajili Ya Watu Wa Ulimwengu Huu Ambao Hawajafikiwa Na Injili, Ukiwataja Kwa Majina

Qatar

Jina la watu

Lugha yao

Idadi yao

Waajemi (Irani)

Farsi, Eastern

65,600

Wanaosema Kiurdu

Kiurdu

28,000




 1985 - 2007

With many thanks to Pastor Dastan Mboera, Dar es Salaaam, Tanzania
and EAPTC Nairobi, Kenya for this revision and translation from the original English.
mboeradsk @ yahoo.com


© Dr Les Norman  The DCI Trust, UK
Permission is granted to provide copies at cost price for study purposes
but not for sale or commercial purposes. Freely you have received, so please freely give.

Support Pages   Index to All Lessons   School of Finances  

World Christian News   
Who Are We?   Site Index

www.dci.org.uk