1985 - 2007

 

65. Kanisa La Utumishi

Gandhi aliliongoza taifa la India kwa huduma na bila kutumia mabavu

Support Pages   Index to All Lessons   School of Finances  
World Christian News   
Who Are We?   Site Index
 

Katika Biblia Yako Soma
1Pet 5:1-4; Eze 34:1-17

Mstari wa Kukariri
Kwa maana Mwana wa Adamu naye hakuja kutumikiwa, bali kutumika, na kutoa nafsi yake iwe fidia ya wengi (Mk 10:45).

Baadaye Zungumzieni Jambo Hili
Linganisha mifumo ya uongozi mahali pa kazi na katika taasisi mbalimbali nchini mwako, na jinsi inavyopaswa kuwa ndani ya Kanisa.

Jambo La Kufanya Kabla Hatujakutana Tena
Enenda ukaoneshe moyo wa mtumishi wa Kristo, ukiwategemeza watu wa chini kabisa kama watoto, watu wa mitaani, waromani, na wasioguswa. Waache jirani na Mungu.

Kazi Ya Kuandika Ya Stashahada
Andika ukurasa mmoja ukielezea tofauti zilizopo kati ya kanisa linaloongozwa na mchungaji, na lingine linaloongozwa na ‘mchinjaji’.

Tafakari Mistari Hii Neno Kwa Neno
Mit 27:23-27
 

Tumia Muda Mfupi Kuubadilisha Ulimwengu

Ombea taifa la Hong Kong. Umiliki wake umerudi mikononi mwa Uchina mwaka 1997.

Ni eneo lenye nguvu kibiashara katika Asia; na lina Wachina na wahamiaji wengine wapatao 6,000,000.

Asilimia 66% ni Tao & Mabudha, asilimia 14% ni Wakristo, ni lango la kimishenari la kuingilia Uchina.

 

Ni Uongozi Au Ubwana?

Kiongozi wa kanisa au umisheni ni tofauti kabisa na viongozi wengine kama wa kisiasa, wa kijeshi, wa biashara au wa kidini. Katika ulimwengu huu mtu mmoja aliyeko juu anadhibiti kila mtu aliyeko chini yake kwa kutumia cheo, shinikizo au hofu ya kupoteza ajira. Yeye, au wabia wake wanapata manufaa makubwa wakati ambapo wafanyakazi wanaweza kuishi katika hali ngumu. Hatushangai kuwepo kwa mapinduzi na migomo. Ni huzuni kwamba baadhi ya makanisa nayo yanatawaliwa kwa mfumo huo. Hali hiyo inasababisha kutokuridhika.
 

Ni Wachungaji Au Wachinjaji?

Mzee mmoja wa busara aliwahi kusema, "Ni watu wa aina mbili tu wanaojishughulisha na kondoo – wachungaji na wachinjaji!

Ni Yupi Mtu Huyu?

Anapenda kuwa wa kwanza. Anawakwepa watumishi wa kweli wa Mungu. Anawasemea wengine maneno maovu na ya chuki. Huwadhibiti watu kanisani, akionesha ubwana wake, ambayo ni namna ya uchawi. Yeye ni Diotrefe, (3Yoh 3-10). Wapo pia wachungaji waovu kwelikweli katika Eze 34:1-6 na Zek 11:15-17.
 

Utawajuaje Wale Wabaya?

Katika mabenki watumishi hujifunza kuzitambua noti bandia kwa kuendelea kushughulika na noti halali. Noti bandia inapowafikia wanaitambua mara moja. Sisi nasi tutaweza kujiepusha na udanganyifu wa viongozi wabaya kwa kujihusisha na viongozi wema.
 

Yesu, Mchungaji Mwema
Y
esu, Simba jasiri wa kabila la Yuda yeye pia ni Kondoo wa Mungu aliye mpole. Kiongozi wa leo anaweza akanguruma kama simba dhidi ya dhambi, na wakati huohuo akawa mnyenyekevu na mpole kwa watu kama mwanakondoo.
 

Njia Ya Mwokozi
Wanadamu kwa kawaida hutawala kwa njia ya uwezo wa jeshi, siasa, fedha au dini; lakini Yesu alichagua namna nyingine kabisa ya uwezo, ambao wengi hawaujui na mara nyingi unadharaulika. Uweza wa ajabu wa unyenyekevu, na huduma ya kujitoa kuwa sadaka.

Katika Mk 8:31, Yesu anatangaza mpango wake mzuri sana wa kuwapata watu wa ulimwengu, kwa kukubali usumbufu; kwa kustahimili dhihaka, fedheha na mateso bila ubishi, na kwa kukubali kukataliwa, kusalitiwa na hata mauti bila malalamiko (Flp 2:6-11) (Yn 12:32). Yesu anazungumza habari ya kufufuka, wanafunzi wake hawaelewi lakini Shetani anaelewa na mara anapinga mpango huo kupitia kwa Petro (Mk 8:32,33).
 

Yesu Ameweka Kiwango

Katika Mk 8:34,35, Yesu anasema kumfuata kuna maana ya mtu kujikana mwenyewe, kukubali mateso ya msalaba na kupoteza maisha kwa ajili ya Bwana. Thawabu ya upotevu kama huo kwa ajili ya Yesu na injili ni uzima halisi!
 

Je, Naweza Kuwa Huyo Kiongozi?

Katika Mk 9:31-39 Yesu anarudia tena mkakati wake wa unyenyekevu na huduma ya kujitoa. La kushangaza ni kwamba wale wafuasi wake walilipokea hilo kwa kuanza kubishana wao kwa wao kuhusu safu ya uongozi miongoni mwao na ni nani atakayekuwa kiongozi wao. Yesu akajibu na kusema kwamba ili uwe wa kwanza ni lazima ujiweke kwenye nafasi ya mwisho na kuwa mtumishi wa wote, hata na watoto na watu wengine walio tofauti.

Je, Naweza Bwana?

Katika Mk 10:32-45, Yesu anaelezea kwa mara ya tatu mkakati wake wa unyenyekevu, na huduma ya kujitoa, na safari hii Yakobo na Yohana wanawania cheo na uweza wa ubwana badala ya huduma. Yesu anajibu na kusema kwamba ni viongozi wa Mataifa pekee ndio wanaowatawala watu, na kwamba haipasi kuwa hivyo miongoni mwa wafuasi wake; hata Mwana wa Mungu hakuja kutumikiwa, bali kutumika na kuutoa uhai wake.
 

Njia Pekee Ya Kwenda Juu Ni Kushuka

Yesu alishuka hadi kwenye mauti na akafufuka. Mkakati wake ulifanya kazi na leo anaongoza mamilioni ya wafuasi wa rangi zote na tamaduni zote, wanaomtii, wanaompenda na kumshukuru. Yesu, akiwa Simba mkamilifu na Mwanakondoo mkamilifu, alitupa sisi mfano mmoja pekee wa uongozi, unyenyekevu na huduma ya kujitoa. Bila kujali wasifu na utamaduni wa kiongozi, atakuwa amefanya vema kunyenyekea, na kuhudumu kwa kujitoa kama alivyofanya Kristo.
 

Je, Linatekelezeka?

Waraka wa kwanza wa Paulo kwa Wathesalonike mlango wa pili, mistari 13 ya kwanza, unaonesha ushuhuda wa uongozi wa kihuduma ukitenda kazi. Paulo alivumilia mateso na matusi, na hakuwa na nia mbaya wala hila. Aliishi kwa kumpendeza Mungu na si wanadamu, hakumfurahisha ye yote na hakuwa na tamaa ya fedha na wala hakuwa mzigo kwa mtu ye yote; lakini alikuwa mpole na mwenye kujali, na kwa kweli akiwa na shauku ya kuishi na wale watu. Alionekana kuwa mtakatifu, asiye na lawama na mwenye haki. Sasa ni nani asiyempenda mtumishi kama huyo?


Na la kufurahisha ni kwamba hata watu wa ulimwengu huu wanatambua uzuri wa uongozi wa kihuduma katika ulimwengu mbaya wa ubwana. Gazeti la TIME la tarehe 9 Mei, 1994 liliripoti kwamba, “Kura huko Ufaransa zinaonesha kwamba kasisi wa watu wasiokuwa na makazi Abbé Pierre ni mtu anayeheshimika sana katika taifa hilo”.
 

Je, Linafanyaje Kazi Siku Hizi?

Andiko la Efe 4:11 linatuambia kwamba Mungu amewaweka mitume, manabii, wainjilisti, wachungaji na walimu kuliongoza kanisa, na ms 12 unatuambia kwamba jukumu lao ni kuwaandaa watu kwa ajili ya huduma, na si kwamba waifanye hiyo huduma peke yao. Lakini kwa vipi?
 

Chagua hapa > 65chart ili uweze kuona mchoro kuhusu somo hili

Umbo La Pembetatu


Katika ulimwengu umbile la pembetatu yule mtu hukaa pale juu. Amri zinatoka juu kwenda chini, na mali kutoka chini kwenda juu. Hata hivyo, katika Ufalme wa Mungu pembetatu ya ulimwengu ni lazima ifanywe kinyume; watu wenye karama sana na wenye uwezo, katika ujumla wao katika uongozi, wakae chini kwenye magoti wakiwa wanategemeza ngazi ya uongozi inayofuata, na ngazi hiyo kutegemeza ngazi nyingine inayofuata, mpaka watu wote wawe wametegemezwa na kuinuliwa karibu zaidi na Mungu.
 

Kwanini Mitume Wakae Chini?

Mitume ni wa kwanza kanisani, sikuzote wakiwa kwenye timu pamoja na wazee, na ni wa kwanza pia katika makanisa ya maeneo (1Kor 12:28) (Mdo 15:2,4,6,22,24) (Mdo 13:1). Yesu alisema nini? Wa kwanza na awe mtumwa wa wote. Na iwe hivyo.

 

Kwa Kumalizia Omba kwa Ajili Ya Watu Ambao Hawajafikiwa Na Injili, Ukiwataja Kwa Majina
 

Somalia

Jina la Watu

Lugha Yao

Idadi Yao

Shambaara (Gosha)

Mushungulu

84,000

Waswahili (Baraawe)

Kiswahili

40,000

Tunni

Tunni

20,000




 1985 - 2007

With many thanks to Pastor Dastan Mboera, Dar es Salaaam, Tanzania
and EAPTC Nairobi, Kenya for this revision and translation from the original English.
mboeradsk @ yahoo.com


© Dr Les Norman  The DCI Trust, UK
Permission is granted to provide copies at cost price for study purposes
but not for sale or commercial purposes. Freely you have received, so please freely give.

Support Pages   Index to All Lessons   School of Finances  

World Christian News   
Who Are We?   Site Index

www.dci.org.uk