1985 - 2007

 

74 (sehemu ya 1) Kanisa La Kimishenari

Wakiwa na Yesu maishani mwao watu walio mbali watapata tumaini, heshima na kusudi

Support Pages   Index to All Lessons   School of Finances  
World Christian News   
Who Are We?   Site Index
 

Katika Biblia Yako Soma
Mdo 11:19-30; 20:1-6

Mstari wa Kukariri
Basi hawa walipokuwa wakimfanyia Bwana ibada na kufunga, Roho Mtakatifu akasema, “Nitengeeni Barnaba na Sauli kwa kazi ile niliyowaitia” (Mdo 13:2).

Baadaye Zungumzieni Jambo Hili
Kama una maono kutoka kwa Mungu, ni watu wachache tu wanaoweza kuangamia. Je, miongoni mwenu kuna maono kwa ajili ya waliopotea?

Jambo La Kufanya Kabla Hatujakutana Tena
Undeni timu na kuchagua kiongozi, na kisha andaeni tukio litakalosababisha kutumika kwa karama na vipawa vilivyoko miongoni mwenu. Fanyeni maombi, wekeni mkakati, na kisha tokeni kwa utekelezaji.

Kazi Ya Kuandika Ya Stashahada
Jifikirie kwamba wewe ni mchungaji na una kanisa la watu 80 na kwamba unataka kuona huduma ya ulimwengu inaanzishwa. Andika malengo yako na kila moja aya yake.

Tafakari Mistari Hii Neno Kwa Neno
Mdo 8:4-8

Tumia Dakika Moja Kuubadilisha Ulimwengu

Ombea taifa la Pakistan. Idadi ya watu ni 145,000,000. Asilimia

97% ni Waislamu wenye siasa kali. Kuna matatizo makubwa ya kijamii na ya kiuchumi.

Kuna mateso kwa Wakristo ambao ni asilimia 2-3%. Watu wengi sana hawajafikiwa na Injili

 

Yafaa sana shirika la kimishenari likazaliwa ndani ya kanisa la eneo moja, likitegemezwa na ushirika wenye maono, na kisha likapita likianzisha makanisa kila liendako. Kanisa lako la eneo moja linaweza likawa kanisa lenye kuubadilisha ulimwengu kwa huduma ya kimataifa, kwa namna ifuatayo:

Kanisa Hilo Ni Nini?
Timotheo Cheni ndiye mchungaji ambaye katika somo la kwanza alifundisha watu 15 kila baada ya miezi miwili na kwa pamoja wamepatikana waamini wapya zaidi ya 100,000. Anasema makanisa yake huko nchini Uchina ni “akiba wa watu walio katika maandalizi kwa ajili ya Agizo Kuu”.

Unahitaji Kufanya Nini Ili Kuanzisha Huduma Kwa Ulimwengu Kanisani Kwako?

Kanisa Linahitaji Maono Ya Mit 29:18
kwa sababu bila maono watu wataangamia. Zaidi ya hayo kiongozi mwandamizi anatakiwa kuutwaa moyo wa Mungu kwa ajili ya ulimwengu wa watu wasiofanana, aende na kujionea mwenyewe, kila mwaka. Litakalomfurahisha yeye litaathiri kanisa lote.

Unahitaji Uongozi Na Umiliki
Watambue wale Mungu anaowainua kwa ajili ya huduma ya ulimwengu katika maombi, matoleo na katika kwenda. Wape majukumu na kuwaweka huru na shughuli za kanisani kwako. Na hilo ndilo lenye maana ya "kuwaacha waende zao" katika Mdo 13:1-3.

Unahitaji Hekima Kwa Ajili Ya Huduma Kwa Ulimwengu
Omba kama Paulo katika Kol 1:9 ili upewe uwezo wa Kimungu wa kuelewa mambo na maarifa.

Ushirika Ni Hekima
Kushirikisha mwili wote kwa upande mmoja, na kufanya kazi kwa ushirikiano na makanisa na misheni nyingine ni jambo jema kwa sababu baraka zimeamriwa kunako umoja. Hakuna kanisa moja peke yake lenye uwezo wa kuubadilisha ulimwengu au hata taifa moja la watu ambao hawajafikiwa.

Unahitaji Kuweka Malengo Na Tarehe

Malengo yanaachilia nguvu na mwelekeo. Kama ukilenga hewa utaipiga hiyohiyo kila mara, na maamuzi yasiyokuwa na tarehe hakika yatachelewa. Unahitaji kuweka malengo ya ~

  1. Maombi ya kuzifunika misheni, ya saa moja au zaidi kila wiki.
  2. Huduma ya kichungaji kwa wale wafanyakazi wa umisheni walioko mstari wa mbele na ambao wanaweza kudhurika kirahisi.
  3. Mafunzo ya kulihami kanisa, angalao kwa muda mfupi kila Jumapili.
  4. Matoleo na makusanyo mengine kutoka vyanzo mbalimbali, kwa malengo ya kueleweka. Matoleo ya imani yameonesha mafanikio makubwa sana. Hapa kila mshirika huweka ahadi ya kumtolea Mungu sadaka kwa ajili ya umisheni kwa mwaka unaofuata kama Mungu atakavyomjalia kutokana na maombi yao. Mwujiza huo ni mbali na mapato yao ya kawaida. Biashara na umisheni vimekuwa kama mbegu mbili katika podo moja.
  5. Kufanya ziara za muda mfupi, kila mwaka kutembelea tamaduni nyingine.
  6. Vipaji vya kimishenari, mathalani matoleo ya chini yawe ni zaka; asilimia 1% ya kanisa wanaweza kwenda. Angalia somo linalofuata.

Unahitaji Mkakati Unaoongozwa na Roho

Katika 1Kor 3:10, Paulo anajitaja kuwa Mjenzi Mkuu, sophos architekton, yaani msanifu mwenye hekima au bwana mipango anayepokea hekima kutoka kwa Mungu kupitia Neno lake na Roho. Hiyo hekima ilikuwa ni nini?

Mkakati Wa Paulo Wa Umisheni
Mkakati wa kimishenari wa Paulo ulikuwa ni kwenda katika njia kuu ziendazo kwenye miji ya watu waabudu sanamu, na kugundua lile kundi la watu ambalo Mungu amelikusudia na kufanya kila linalowezekana kuhakikisha kwamba wameokolewa, wamekomaa na wanawahudumia wengine. Msingi wa misheni aliouweka ulikuwa na sehemu kuu mbili ~

Makanisa Mama
Katika Biblia tofauti pekee tunazoziona kati ya makanisa ni zile za kijiografia kama vile makanisa ya Yerusalemu, Antiokia, Filipi, na Efeso ambayo yalizaa makanisa mengine na kuyategemeza. Aidha yalijihusisha na shughuli za kimishenari katika kueneza injili. Antiokia lilikuwa ndilo kanisa mama la Paulo. Alipelekwa kutokea pale na kurejea tena pale pale katika huduma yake ya kimishenari.

Timu Za Kitume
Neno “kitume” hapa lina maana ya kutumwa na Mungu, na si lazima kuongozwa na mtume kama ambavyo hata Paulo hakutambuliwa hivyo kwa wakati ule. Mungu alipomwita kwenye umisheni aliunda timu ndogo ya kitume ya watu watatu ikiwa na mkakati wa wazi wa kuwaendea wasiofikiwa bado, Mdo 13:1. Kuanzia hapo huo ukawa ndio utendaji wake, na katika Mdo 20:4 watu kutoka makanisa mbalimbali wanashirikiana naye katika shughuli za umishenari.

Kanisa Na Umisheni Ni Mapacha

Kanisa lilikuwa ni kanisa na umisheni ulikuwa ni umisheni tangu mwanzo. Timu ya kimishenari ilikuwa na mamlaka ya kanisa la eneo moja; na kwa hakika lilikuwa ni kanisa linalosafiri. Paulo alipoondoka alijisimamia mwenyewe, akitegemezwa, na wala si kudhibitiwa na kanisa la Antiokia, Yerusalemu au Filipi. Timu ilijitosheleza kiuchumi. Walipokuwa barabarani, walijitawala, walijitafutia fedha kwa mahitaji yao, na walijizaa wenyewe kwa maana ya kuanzisha makanisa mapya, shule na timu za kimishenari. Lengo ni moja, lakini njia za utekelezaji ni mbili.

Hatua Zilizopendekezwa Pamoja Na Uongozi Wa Mungu

  1. Timu iende, ione, ipeleleze na kurudi.
  2. Timu ifanye maombi sana, iende tena, ifanye ibada mahali husika, izungumze na watu na kujifunza habari zao, na kisha irejee.
  3. Safari hii timu iende na kukaa. Kwanza kabisa wanatimu wajifunze njia za wenyeji wao na utamaduni wao, ili pawepo na urahisi wa mawasiliano. Halafu waanze kushuhudia na waamini wapya waanzishe kanisa.
  4. Timu iwafanye waamini wapya kuwa wanafunzi; na kuteua viongozi kutoka miongoni mwao haraka iwezekanavyo. Kisha kanisa hilo litume timu ya kimishenari kwenda kijiji cha jirani; na kwa hiyo kanisa hilo limekuwa kanisa la kimishenari tangu siku ya kwanza ya kuanzishwa kwake.
  5. Hatua ya mwisho ni kukabidhi kanisa hilo jipya kwa wenyeji, na timu kuhamia mahali pengine.

Angalia pia somo la 64; na la 74 sehemu ya 2

 

Kwa Kumalizia Omba Kwa Ajili Ya Watu Ambao Hawajafikiwa Na Injili, Ukiwataja Kwa Majina

Uganda

Jina la Watu

Lugha Yao

Idadi Yao

Lulba

Luluba

15,000

 




 1985 - 2007

With many thanks to Pastor Dastan Mboera, Dar es Salaaam, Tanzania
and EAPTC Nairobi, Kenya for this revision and translation from the original English.
mboeradsk @ yahoo.com


© Dr Les Norman  The DCI Trust, UK
Permission is granted to provide copies at cost price for study purposes
but not for sale or commercial purposes. Freely you have received, so please freely give.

Support Pages   Index to All Lessons   School of Finances  

World Christian News   
Who Are We?   Site Index

www.dci.org.uk