1985 - 2007

 

77. Habari Za Ufalme

 

Support Pages   Index to All Lessons   School of Finances  
World Christian News   
Who Are We?   Site Index
 

Katika Biblia Yako Soma
Mwa 1; Ufu 20:11-21:5

Mstari wa Kukariri
Naye atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena; kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita. Na yeye aketiye juu ya kile kiti cha enzi asema, ‘Tazama nayafanya yote kuwa mapya…’ (Ufu 21:4,5).

Baadaye Zungumzieni Jambo Hili
Unalopaswa kuwania ni mategemeo ya baadaye yenye utukufu na yenye uhakika kutoka kwa Mungu kwa ajili yako milele.

Jambo La Kufanya Kabla Hatujakutana Tena
Tafuta kibali cha kutembelea mashule, vyuo na vyuo vikuu ili kuwashirikisha mtazamo wa ulimwengu wa Kikristo, uliopita, uliopo na ujao.

Kazi Ya Kuandika Ya Stashahada
Andika taarifa ya ukurasa mmoja ukielezea maana ya kile Ebr 6:4,5 inachosema ni kuonja karama na uweza. Je, dhifa kamili inaweza kufananaje?

Tafakari Mstari Huu Neno Kwa Neno
Ufu 20:15

Tumia Dakika Moja Kuubadilisha Ulimwengu

Ombea taifa la Nepal. Idadi ya watu ni 21,000,000. Asilimia 

89% ni Wahindu; Asilimia 0.5% tu ni Wakristo; mwaka 1960 kulikuwa na waamini 25, sasa wamefikia 50,000.

 

Chagua hapa > 77chart ili uweze kuona michoro kuhusiana na somo hili

Igundue Asili Yako

Unaweza ukadhani kwamba Ukristo ni kitu kigeni sana hapa duniani, au kwamba ni dini ya nchi za magharibi ambayo inaweza kuwa ya maana zaidi kuliko imani nyingine za kienyeji. Mawazo hayo si sahihi hata kidogo. Sasa unakaribia kuugundua ukweli kuhusu utambulisho wako na kuona kuwa wewe ni sehemu ya familia kubwa yenye historia inayoanzia kabla ya kuwepo wakati, na itakayoendelea hadi wakati ujao wa utukufu. Hapa pana maelezo mafupi:

1. Kabla Ya Historia

Kabla historia haijakuwepo ilikuwa ni umilele tu, (Zab 90:2). Si mengi yanayofahamika lakini Biblia inadokeza au kutoa nuru (Zab 2:7). Katika Eze 28:12-19 na Isa 14:12-20, Biblia inatoa maelezo kumhusu Lusifa au Shetani.

2. Zama Hizi

Zama hizi zilianza kwa Mungu kuumba mifumo ya sayari ikiwemo dunia, Adamu na Hawa, na wala si kwa mageuko yatokanayo na mlipuko mmoja mkubwa ambao wanasayansi wanadhani ndio ulioleta uumbaji. Baada ya anguko la mwanadamu, zama hizi hadi leo zinawakilishwa na orodha kwenye chati inayoitwa, kifo,dhambi na Shetani.

Matukio Ya Kwanza Katika Historia Ya Mwanadamu ni…
Uumbaji, dhambi, anguko la mwanadamu, kifo, ahadi ya Mungu ya kuweka mambo sawa, kuzaliwa kwa uadui dhidi ya Shetani na mwanzo wa harakati zake za kutaka umaarufu hapa ulimwenguni. Wanadamu wamegawanyika katika makundi mawili: Wakaini wanajulikana kwa fujo zao na kutokumcha Mungu; na Wasethi kama Henoko ni wacha Mungu. Hata hivyo panatokea uvamizi wa kiroho; yaani ndoa kati ya roho na wanadamu. Hali hiyo inasababisha mgogoro mkubwa wa dhambi hapa duniani (Mwa 1-5).

Nuhu, Gharika Na Agano
Mwa 6-11:9. Hata hivyo dhambi inakaa: Mwa 9:20-22, na mara inabadilika kuwa ibada ya sanamu na Mungu anatoa hukumu penye mnara wa Babeli, ambapo unakuwa mwanzo wa mataifa na tamaduni: Mwa 11:1-9.

Ibrahimu
Katika Mwa 11:27-12:1 na kuendelea, Mungu anaamua kumgeukia mtu mmoja, Ibrahimu, ambaye Mungu amemkusudia awe baba wa kundi jipya la watu, watu wa Mungu.

Isaka Na Yakobo
Mwana wa Ibrahimu na mjukuu wake wanarithi ahadi ileile kama alivyoipokea (Mwa 12:1-3), na inapitishiwa kwa Yusufu hadi Misri kwenye miaka 400 ya utumwa. Soma Mwanzo 21 hadi Kutoka na kisha somo la 29.

Musa Hadi Israeli Na Yuda
Kwa mkono wa Mungu Musa aliwaokoa taifa zima kutoka Misri na wakakutana na Mungu pale Sinai (Kutoka 19 na 20; na somo la 29). Na ingawaje kamwe hawakuwa ufalme wa makuhani na taifa takatifu, lakini waliwakilisha imani katika Mungu mmoja aliye hai kwa miaka 1,500 kila mara wakiutafuta ufalme ujao (Waamuzi-Malaki).

Yesu
Tangazo la jambo jipya kutoka kwa Mungu lilimjia mwanamwali mmoja katika familia ya kikulima katika mji wa kaskazini.  Kwa wachungaji ambao wala hawakuwa na haki ya kutoa ushahidi katika mahakama ya kisheria na pengine, la kushangaza, hata kwa mamajusi. Wanatheolojia walikuwa wapi? Na waandishi wa habari je? Je, walikuwa wapi watu wa dini waliokuwa na nguvu na ambao wangeweza kuhakikisha kwamba Mwana wa Mungu anawarejesha kwa nguvu wafuasi wa dini ya Kiyahudi wamrudie Mungu na wito wake mtakatifu? Mungu alijua kwamba nguvu za giza zinakaa ndani yao wanaoidhibiti jamii. Kwahiyo injili hii, yaani mtoto huyu, walikabidhiwa wakulima, wachungaji na mamajusi waliokuwa wanatafuta jambo ng’ambo ya nyota.

Yesu, Ni Wa Kwanza Katika Kizazi Kijacho
Yohana Mbatizaji anatangaza kwamba ufalme umekaribia, mwisho wa Agano la Kale. Yesu anahubiri habari njema kwamba ufalme umekaribia, na anafundisha namna ya kuuingia. Yesu anawatuma wafuasi wake kwenda kusema yayo hayo, na miujiza inathibitisha kuwasili kwa Ufalme wa Mungu. Yesu, kwa kujiamini, anatangaza sheria za baadaye za ufalme huo na kufundisha namna watu watakavyoishi humo, na majaliwa yao, kwa kutumia mifano; kwamba si suala la matumani bali ndiyo kweli yenyewe. Anaahidi kwamba ufalme wake utavuka mipaka ya kifo chake na anataka tuombe ili kwamba ufalme wake uzidi kuja. Maana yake hapa ni kwamba Yesu anatangaza vita dhidi ya ufalme wa Shetani. (Mt 3:2; 5:20; 7:21) (Yn 3:3) (Mt 10:7; 12:28) (Mt 5, 6 na 7) (Mt 13:11) (Lk 22:30; 11:2) (Mt 12:26) (1Yn 3:8).

Msalaba Unasafisha Njia
Adui amenyang’anywa silaha (Kol 2:15), lakini bado yupo na ataendelea kuwa wa hatari hadi Yesu atakaporudi.

3. Kizazi Kipya Chaanza Kuingia

Ufufuko (Yn 20 – 21)

Shule ya kwanza ya Biblia (Mdo 1:3)

Ahadi ya Roho Mtakatifu (Mdo 1:5)

Mkakati wa muda mrefu (Mdo 1:8)

Kipindi cha Kanisa Chaanza

Kipindi cha utukufu wa Kristo uliositirika.

Sisi tunaonja tu, karamu yenyewe bado, ambayo kwenye orodha katika chati inaitwa ‘Ladha’.

 

Roho Mtakatifu ndiye anayetutia nguvu katika mapambano falme mbili hizi zinapokwaruzana na hali hiyo itaendelea hadi Yesu atakaporejea (Mdo 2:1-4). Shetani anapata pingamizi kubwa kila mara mgonjwa anapoponywa, kila mara pepo linapotolewa, kila mara mwenye dhambi anapookoka; kila mara watu wa rangi tofauti wanapoishi kwa pamoja kwa maelewano; kila mara ulafi unapodhihirika na kuadhibiwa; kila mara familia zinapoishi katika utakatifu na usafi. Shetani huja kuiba, kuua na kuharibu, bali Yesu hutuletea uzima tele.

 

Kristo Anakuja Mara Ya Pili Kama Mfalme

Kipindi cha utukufu dhahiri wa Kristo.

Ufufuko wa kwanza, (1Kor 15:35-57).

Shetani atafungwa na Yesu atatawala hapa duniani kwa miaka 1000 na baada ya hapo Shetani atafunguliwa na watu watamfuata tena wakifanyika mateka wa dhambi (Ufu 20:1-8).

 

Ufufuko Wa Pili

Hukumu ya mwisho na kufunguliwa kwa vitabu mbele ya kiti cha enzi cha Mungu. Kisha kutupwa kwenye ziwa la moto; mauti, kuzimu, Shetani na wafuasi wake, na wale wote ambao majina yao hayakuandikwa kwenye kitabu cha uzima (Ufu 20:11-15).

4. Ufalme Wa Mungu Unakuja Kikamilifu

Nchi mpya na mbingu mpya na utawala wa haki wa Mungu vitadumu milele. Angalia orodha ya mwisho kwenye chati kisha umshukuru Mungu kwa kukuleta kwenye ufalme wake salama.

 

Kwa Kumalizia Omba Kwa Ajili Ya Watu Wa Ulimwengu Ambao Hawajafikiwa Na Injili, Ukiwataja Kwa Majina

Mwungano Wa Falme Za Kiarabu

Jina la Watu

Lugha Yao

Idadi Yao

Pashtun, Western (Pushtun, Pathan, Afghan)

Pashto, Western

38,100

Yemeni Arab

Arabic, Ta'izzi-Adeni

15,000

 




 1985 - 2007

With many thanks to Pastor Dastan Mboera, Dar es Salaaam, Tanzania
and EAPTC Nairobi, Kenya for this revision and translation from the original English.
mboeradsk @ yahoo.com


© Dr Les Norman  The DCI Trust, UK
Permission is granted to provide copies at cost price for study purposes
but not for sale or commercial purposes. Freely you have received, so please freely give.

Support Pages   Index to All Lessons   School of Finances  

World Christian News   
Who Are We?   Site Index

www.dci.org.uk