1985 - 2007
82. Ufalme Wenye Umoja
Mtu mmoja mashuhuri Bw. George Bernard Shaw aliwahi kuulizwa, "Ulimwengu una tatizo gani?" Alijibu kwa kuliandikia gazeti la London Times maneno haya, "Kuhusu swali mliloniuliza, ‘Ulimwengu una tatizo gani?’ Mimi ndiye. Wenu, G.B. Shaw”
Support Pages
Index to All Lessons School of Finances
World Christian News
Who
Are We? Site Index
Katika Biblia
Yako Soma
Yn 17 na
Mdo 10
Mstari wa
Kukariri
Kuna mwili mmoja, na
Roho mmoja, kama na mlivyoitwa katika tumaini moja la wito wenu. Bwana mmoja,
imani moja, ubatizo mmoja. Mungu mmoja, naye ni Baba wa wote aliye juu ya yote
na katika yote na ndani ya yote (Efe 4:4-6).
Baadaye
Zungumzieni Jambo Hili
Kila
mmoja apeleleze moyo wake ili kuona kama kuna namna ya chuki bila sababu, mawazo
yaliyojengeka kabla ya kuona, na mila; kisha ungama na kutubu kwa ajili ya wale
waliotakaswa na Mungu bali wewe ukawaita najisi. Ni nani akina Kornelio katika
eneo lako?
Jambo La
Kufanya Kabla Hatujakutana Tena
Wiki hii
watembelee akina ‘Kornelio’ wengi kadiri uwezavyo ili kuwatia moyo.
Kazi Ya
Kuandika Ya Stashahada
Katika
ukurasa mmoja andika mapendekezo yako kuhusu ni nini kifanyike katika eneo lako,
ili kupitia umoja wetu, watu wapate kuamini.
Tafakari
Mstari Huu Neno Kwa Neno
Efe 4:3
Tumia Dakika Moja Kuubadilisha Ulimwengu
Ombea taifa la Colombia. Idadi yao ni 35,000,000.
Asilimia 93% ni Wakatoliki; na asilimia 3.1% ni wa madhehebu ya Kiinjili. Ni maarufu kwa madawa ya kulevya na fujo. Kuna kiasi fulani cha ukuaji wa kanisa.
1. Je, Maombi Ya Yesu Yatajibiwa?
Yesu aliomba ili kwamba sisi tupate kuwa wamoja kama vile Mungu alivyo Mmoja, angawa ni nafsi tatu katika Umoja huo. Mungu anataka kundi lake pia liwe moja, chini ya Mchungaji mmoja, ingawa kuna hali ya kuwa anuwai katika kundi hilo. Kebehi kubwa zaidi tunayoipata kutoka kwa watu ni kanisa letu kuwa na migawanyiko mingi; na vilevile hatuna udhuru kwa kupuuzia injili. Kwa ujumla watu hawana tatizo kubwa na Mungu, tatizo linaweza kuwa kwetu sisi, namna tunavyomtambulisha kwa mataifa. (Yn 17:11; 21:22; 10:16).
Je, Uinjilisti
Wako Unafanya Kazi?
Wakati
mwingine tunatoa kiasi kikubwa sana cha fedha kugharamia shughuli za umisheni,
lakini hatutilii maanani mkakati wa uhakika zaidi wa uinjilisti.(Yn 17:21-23 na
Yn 13:34,35).
2. Ahadi Ya Kuwa Wamoja
Kuongezeka Kwa Upako
Na Chakula
Katika
1Nya 12:38,39; 2Sam 2:4 wakati Daudi na wale watu wenye nguvu walipokuwa wamoja.
Baraka Zilizoamriwa
Mlima Sayuni ni mahali
pakame na penye mavumbi, lakini ndugu wanapokaa kwa umoja wanakuwa kama Sayuni
inavyofurahia kila siku maji ya uzima yanayoufanya Mlima Hermoni kuwa maarufu.
Mafuta kwa ajili ya uponyaji na kwa ajili ya upako hutiririka kutoka kichwani na
kuufikia mwili wote (Zab 133).
Kwanini Tunapendelea
Kulaaniwa?
Baraka za
jinsi hiyo haziwezi kupatikana pale tunapong’ang’ania kugawanyika na kuwa na
madhehebu mengi kila moja likiwa na makanisa yake, vyuo vyake, agenda zake, na
shughuli zake za umisheni. Udhehebu unapingana kabisa na sala ya Yesu, na
unajenga kuta za ubaguzi zilizoendelezwa na kudumishwa na vizazi vingi pasipo na
makasisi wa kanisa. Kila anayeshabikia udhehebu ni mwasi mbele za Mungu.
3. Kwanini Haya Hutokea?
Watu Walioanguka
Ni vema
tuelewe kuwa hata wakristo wanaweza kuwa na ubinafsi, mashindano katika tamaa ya
makuu, uchu wa madaraka na kujijengea himaya binafsi, kama hali hii haitazuiwa.
Mkakati Wa Kishetani
Shetani
ameingia kanisani siku nyingi ili aendeshe vita akiwa ndani ya kanisa badala ya
kufanya tu mashambulizi akiwa nje (Lk 11:17).
Twajenga Kuta Na
Wala Si Misingi
Kumbuka
maneno haya kwa ajili ya umoja:
· kweli zisizokuwa na shaka,
· tafsiri
· mafundisho
· mawazo binafsi
Tunapoangalia kweli zisizokuwa na shaka kama vile imani kwamba Mungu yupo, dhambi ya mwanadamu, Kristo kama Mwokozi, na uzima wa milele; sisi ni wamoja katika mambo hayo. Kweli zisizokuwa na shaka ni hoja inayokubaliwa nasi sote na hasa tunapokabiliana na dini potofu kwa pamoja.
Lakini tunapoendelea na mtindo wa kuhubiri tafsiri zetu wenyewe kwa mstari fulani katika Maandiko, au mafundisho yetu wenyewe kutoka kwenye mistari kadhaa ya Maandiko, au mbaya zaidi tunapong’ang’ania kautamaduni ketu wenyewe au mawazo binafsi na hisia zetu hata kama si sahihi, basi tujue kwamba tunajenga kuta zinazotugawa.
4. Kuwa Wamoja
Tunapaswa kumshukuru Mungu kwamba katika maeneo mengi ya ulimwengu huu kuna mvumo mpya na mzuri, wa upepo kutoka kwa Mungu. Je, tunaweza kufanya nini ili kusaidia kuleta uponyaji kwa mwili wa Kristo uliopasuka na kugawanyika?
Toba
Mtu mmoja
mashuhuri sana Bw. George Bernard Shaw aliwahi kujiuliza, "Hivi ulimwengu una
tatizo gani?" Alijijibu swali lake mwenyewe kwa kusema, "Mimi ndiye." Tofauti
iliyopo kati ya maneno mawili ya Kiingereza UNITED(-iliyounganika) na
UNTIED(-iliyofunguliwa, mathalani mzigo wa kuni) ni mahali ilipo
herufi I.(Na herufi I inaposimama yenyewe katika lugha ya Kiingereza
ina maana ya mimi). Mara zote jibu linaanzia kwangu na mahali nilipo
kuelekea kwako.
Tulinde Sana Kile
Alichotupa Mungu
Efe 4:3
inatuagiza kuuhifadhi umoja wa Roho katika amani. Kuhifadhi kitu maana yake ni
kwamba kitu hicho kilishakuwepo, kwa hiyo sisi tumeunganika sana kuliko
tunavyodhani, ingawa yapo mambo mengi yanayotupa changamoto. Umoja wa Roho ni
umoja unaoletwa na Roho Mtakatifu, na wala hauletwi na kufanana kwetu katika
mafundisho, utamaduni, mtindo wa maisha au taratibu za ibada.
Tubu Kwa Ubaguzi
Binafsi
Katika
Mdo 10: 9-16, Mungu alimwonesha Petro katika maono bustani ya wanyamapori
ikishuka kutoka mbinguni juu ya kitambaa. “Petro amka, chinja ule.” Petro
Myahudi yule akajibu “Hasha Bwana, umekosea. Ninazijua fika sheria za dini
yangu; siwezi kula hao wanyama.”
Na katika kuufikisha ujumbe Mungu anampa Petro changamoto mara tatu kuhusiana na ubaguzi wake, mawazo yake ya awali, ukaidi wake, ubinafsi wa dini yake na wa kabila lake. Kwanini? Alikuwa anamwandaa kwa ajili ya uamsho mahali ambapo hakupatazamia, mahali ambapo asingeweza kwenda kutokana na ubaguzi huo. Ni nyumbani kwa Mmataifa mmoja ambako Mungu alikuwa akimsubiri (Mdo 10:17-48).
Ni Najisi - Au
Hajulikani Na Hapendwi?
Tunahitaji kuwafikia akina ‘Korinelio’ wa kileo ambao yawezekana tamaduni zetu
zimetofautiana, na pengine hatuwapendi na tusijue kwamba Mungu anawajali. Na,
je, ni watu wangapi wa rangi tofauti, dini na madhehebu tofauti ambao wanataka
kumpenda Mungu wasiyemfahamu? (Mit 30:1-6).
5. Kufanyika Ufalme Uliounganika
Wakristo wanaweza kuwa watu wa mapokeo, au wana karismatiki, au wenye msimamo mkali; lakini, je, tunaweza kukua pamoja ili ulimwengu upate kuamini?
Tunaweza Kufanya Nini?
Kwa Kumalizia Omba Kwa Ajili Ya Watu Wa Ulimwengu Ambao Hawajafikiwa Na Injili, Ukiwataja Kwa Majina
Vietnam |
||
Jina la Watue |
Lugha Yao |
Idadi Yao |
Roglai, Southern |
Roglai, Southern |
20,000 |
Tai, Red (Thai Deng) |
Tai Daeng |
100,000 |
1985 - 2007
With many thanks to Pastor Dastan
Mboera, Dar es Salaaam, Tanzania
and EAPTC Nairobi, Kenya
for this revision and translation from the original English.
mboeradsk @ yahoo.com
© Dr Les Norman The DCI Trust, UK
Permission is granted to provide
copies at cost price for study purposes
but not for sale or commercial
purposes. Freely you have received, so please freely give.
Support Pages
Index to All Lessons School of Finances
World Christian News
Who
Are We? Site Index
www.dci.org.uk