1985 - 2007

 

83. Ni Ufalme Au Maafa

Jumbe za nyakati za mwisho kutoka mbinguni

Support Pages   Index to All Lessons   School of Finances  
World Christian News   
Who Are We?   Site Index
 

Katika Biblia Yako Soma
Ufunuo 14

Mstari wa Kukariri
”…Mcheni Mungu, na kumtukuza, kwa maana saa ya hukumu yake imekuja. Msujudieni yeye aliyezifanya mbingu na nchi na bahari na chemchemi za maji” (Ufu 14:7)

Baadaye Zungumzieni Jambo Hili
Jadilini jinsi mnavyowaona wale wapanda farasi wanne katika Ufunuo wanavyopita duniani katika siku za maisha yenu.

Jambo La Kufanya Kabla Hatujakutana Tena
Andika makala ukiwaonya watu kuhusu unabii wa Biblia kuhusiana na kuanguka kwa biashara, na kuyapeleka kwenye redio na magazetini. Usitumie mbinu za vitisho.

Kazi Ya Kuandika Ya Stashahada
Andika ukurasa mmoja wa mapendekezo ya namna bora ya kumfanyia Bwana ibada makanisani mwetu tukizingatia njia za kumletea yeye utukufu.

Tafakari Mistari Hii
Ufu 19:1,2

Tumia Muda Mfupi Kuubadilisha Ulimwengu

Ombea taifa la Eritrea. Idadi ya watu ni 4,000,000 katika makabila tisa. Kumekuwako na miaka 30 ya vita na njaa. Asilimia 50% ni Waislamu; na asilimia 40% ni Orthodox. Wana changamoto kubwa ya kujenga upya taifa lao.  

 

Watu wengi wanaamini kwamba sasa tupo katika siku za mwisho kabla Yesu hajarejea kama Mfalme. Hakika hakuna siku baada ya leo. Kumalizika kwa mwaka 1999 na kuingia 2000 na kuanza kwa milenia mpya kuna umuhimu mkubwa wa kinabii kwa watu wengi; na hata kutimia kwa mwaka wa 6000 katika kalenda ya Kiyahudi kuna umuhimu mkubwa kwa wengine pia. Wanasayansi wanahofia uharibifu wa mazingira, migogoro ya kisiasa inaendelea, na kiroho sisi tunajua ya kwamba dhambi, uhalifu, udhalimu na kukosekana usawa havitadumu milele. Kuna jambo linalokwenda kutokea.

Wapanda Farasi Wa Ufunuo

Katika Ufunuo 6:1-8 tunajifunza habari za wapanda farasi wanne watakaoiendesha dunia. Sauti za kwato zao hazikuwahi kueleweka vizuri. Aliyempanda farasi mweupe ni Yesu, naye atashinda mioyo ya wanadamu (Ufu 19:11).

Ni jambo la kushukuru kwa kuwa Biblia inasema kwamba dhambi inapoongezeka, neema nayo huzidi.(Rum 5:21). Tunakwenda kukutana na malaika watatu wenye jumbe zinazoeleweka kutoka kwa Mungu kuhusiana na nyakati za mwisho. Inawezekana ni viongozi wa Kikristo watakaousikizisha ulimwengu kwa sababu katika Ufunuo ule mlango wa pili neno malaika linamaanisha viongozi wa makanisa.

1. Malaika Wa Kwanza

Anahubiri Injili ya milele kwa kila taifa, na kabila na lugha kama yenye umuhimu wa kwanza mbele za Mungu. Malaika huyu ana jumbe tatu:

  1. Katika ulimwengu wenye hofu – mche Mungu peke yake.
  2. Mtukuze yeye. Katika kipindi hiki cha maendeleo makubwa ya maarifa, madawa na sayansi, Mungu anatarajia kupewa heshima na shukrani kwa rehema zake.
  3. Mwabudu yeye peke yake, aliye mwumbaji na wala si vilivyoumbwa naye. Na mara nyingi ibada huishia tu kuimba kanisani. Tunaweza pia kumwabudu Mungu kwa kushirikiana naye katika kuipa kipaumbele huduma ya kukamilisha Agizo Kuu (Rum 1-3).

2. Malaika Wa Pili

Huyu anasema, ‘Umeanguka Babeli’ (Ufu 14:8). Babeli ni nyumbani kwa mapepo na roho chafu na kwa uchawi wao huwapotosha mataifa na kuwatia wendawazimu hata wakawaua watakatifu wengi. Wafalme, watawala na wafanyabiashara wakubwa wanafanya uasherati na Babeli, kwa kuwa Babeli unawapa maisha ya anasa na utajiri na kuwawezesha wafanyabiashara hao kuwa watu wakubwa. Babeli unawatimizia watu tamaa zao za mali na ufahari. Ni biashara ya ulimwengu katika vitu vya kifahari wakati watu kwa mamilioni wana shida ya chakula na hivyo kulazimika kujifanyia biashara miili yao, ya watoto wao na nafsi zao (Ufu 17 na 18).

Maangamizi Katika Saa Moja!
Katika muda wa saa moja utaangamizwa! Je, hili linawezekana? Lakini Bwana ameshatoa maonyo mengi katika siku za karibuni. Kwa mfano himaya ya Maxwell imeanguka. Mabenki ya Kijapani yameshindwa. Bidhaa na hisa katika mtandao wa kompyuta hukua na kuporomoka. Je, unaikumbuka taasisi yenye sifa mbaya iliyojulikana kwa jina la Black Wednesday (Jumatano Nyeusi) mwaka 1992? Walanguzi wa kimataifa waliharibu thamani ya pauni ya Uingereza na sarafu nyingine za Ulaya. Wawekezaji wengi, wakiwemo wachungaji walipoteza katika kipindi cha saa moja tu mamilioni ya pauni katika Soko la Hisa la London. Uchumi wa nchi kama Korea na Brazili uliporomoka katika kipindi cha siku chache tu.

Ondokeni Kwake Enyi Watu Wangu
Haya yalikuwa ni maonyo tu kutoka mbinguni kwa ajili ya watu wa Mungu ili waitii amri ya Ufu 18:4. Tunatakiwa kujikabidhi kwa Mungu sisi pamoja na mali zetu, la sivyo tutazipoteza wakati mfumo wa ulimwengu utakapohukumiwa. Wakristo wanapaswa kuhakikisha kwamba akiba zao, vitega uchumi vyao na hisa zao ziko katika mikono salama, na si mahali pasipokuwa salama (Hag 2:6,7) (Yer 51:6,7). Babeli utaanguka.

3. Malaika Wa Tatu

Ujumbe wa malaika wa tatu ni wa kuwaandaa watu wa Mungu ili wasije wakakubaliana na utaratibu wa yule mnyama na pia wasije wakaipokea alama yake ili kwamba waweze kununua; la sivyo wataipokea ghadhabu ya Mungu (Ufu 14:9; 13:11-17).

Huyo Mnyama Ni Nani?
Huyo ni kiongozi ajaye mwanasiasa mwenye hadhi ya kilimwengu. Atakuwa mwenye nguvu na ushawishi mkubwa naye ataongoza kwa uwezo wa nguvu za giza zitakazodai kuabudiwa.

Na Hiyo Alama Ni Nini?
Teknolojia ya kuweka alama tayari ipo katika nchi za Magharibi na inasubiri tu kukubalika na watu wengi. Kifaa cha elektroniki kitakachowekwa kwenye mkono au kichwani ni wazo zuri sana la kukabili uhalifu na kuondoa fedha kwenye mzunguko.

Wakristo wanatakiwa kugundua imani katika Mungu kwa ajili ya mahitaji yao (Isa 55) pamoja na kuwa na mtindo wa maisha usiokuwa na tamaa ya vitu yakinifu, Mdo 2:42-47, ili kwamba makubaliano na huyo mnyama yaweze kuepukika. Na hilo lina maana kwamba watu wa Mungu wanapaswa kuwa na subira na uvumilivu ingawa pia baadhi yao wanaweza kupatwa na mateso na hata kifo. Na hilo lina maana vilevile kwamba mtu wa Mungu atatakiwa kufa kila siku kutokana na dhihaka na kutengwa.

Ni Mambo Ya Kukisia Tu, Au Ni Unabii?
Utayafanyia nini yote haya? Soma Zekaria 1:4-6 kabla hujajibu.

4. Namna Mbili Za Mavuno Katika Dunia

Uvunaji Wa Kwanza Utafanywa Na Yesu
Yesu anaamuru uvunaji wa duniani wa watu wa Mungu watakaoishi naye milele (Ufu 14:14-16) (Dan 7:13).

Uvunaji Wa Pili Ni Mauti Ya Milele
Huu utafanywa na malaika anayehusika na moto wa hukumu na uharibifu kwa hao wote waliokataa kumcha Mungu, kumtukuza,  na badala yake wakapendelea kuishi katika ufalme wa Shetani. Ni mavuno ya shinikizo la mvinyo wa hasira ya Mungu ya kutisha (Ufu 14:11, 17-20) (2Pet 3:12).

Sasa tunaelewa umuhimu wa ujumbe wa yule malaika wa kwanza kutoka mbinguni wa kukamilisha Agizo Kuu. Tutahitajiana katika nyakati zinazokuja. Kwa wakati huu tunapaswa kujiwekea hazina zetu mbinguni kwa kuwekeza maisha yetu katika kazi ya Mungu kwa ajili ya waliopotea na walio maskini, tukitumia utajiri wa kidunia kupata marafiki kwa kupeleka injili ya Ufalme kwa kila taifa (Mt 6:20) (Lk 16:9).

 

Kwa Kumalizia Omba Kwa Ajili Ya Watu Wa Ulimwengu Huu Ambao Bado Hawajafikiwa Na Injili, Ukiwataja Kwa Majina
 

Yemen

Jina la watu

Lugha Yao

Idadi Yao

Mahra (Mehri, Mahri)

Mahri

294,000

Malay

Malay

28,000

Persian (Irani)

Farsi, Western

14,000

  




 1985 - 2007

With many thanks to Pastor Dastan Mboera, Dar es Salaaam, Tanzania
and EAPTC Nairobi, Kenya for this revision and translation from the original English.
mboeradsk @ yahoo.com


© Dr Les Norman  The DCI Trust, UK
Permission is granted to provide copies at cost price for study purposes
but not for sale or commercial purposes. Freely you have received, so please freely give.

Support Pages   Index to All Lessons   School of Finances  

World Christian News   
Who Are We?   Site Index

www.dci.org.uk