1985 - 2007

 

9. Ponya Wagonjwa
Mwendee Yesu unapomhitaji sana

Support Pages   Index To All Lessons   School of Finances  
World Christian News   
Who Are We?   Site Index
 

Kwenye Biblia Yako Soma
Zaburi 103  &  Mathayo 8: 1-17

Mstari Wa Kukariri
Yeye mwenyewe alizichukua dhambi zetu katika mwili wake juu ya mti; ili, tukiwa wafu kwa mambo ya dhambi, tuwe hai kwa mambo ya haki; na kwa kupigwa kwake mliponywa (1Pet 2:24).

Baadaye Zungumzieni Jambo Hili 
Angalia orodha ya watu wanaoombea wagonjwa. Je, upo mahali gani katika orodha hiyo?
Je, kinachokuzuia kuhudumu sasa ni nini?

Jambo La Kufanya Kabla Hatujakutana Tena
Mwombe Mungu akuelekeze kwa wagonjwa na hakikisha unatii anapokuongoza kukutana na mtu, kumwona au kumsikiliza, hata kama ni mgeni. Waendee, na hata kama hawataamini lakini bado unaweza kuwaombea ili waponywe kwa jina la Yesu.

Kazi Ya Kuandika Ya Stashahada
Kutoka katika vitabu vya Injili andika orodha ya matukio yote ambapo Yesu alihudumia wagonjwa mbalimbali, katika mazingira tofauti, na mbinu mbalimbali alizotumia.

Tafakari Mistari Ifuatayo Neno Kwa Neno
Mdo 14: 8-10

Tumia Dakika Moja Kuubadilisha Ulimwengu

Ombea taifa la Urusi. Idadi ya watu: 154,000,000.
Baada ya kuanguka kwa Ukomunisti kumejitokeza ugumu wa maisha na uhalifu.

 

Hakikisha umewafundisha wengine somo hili.
Kila mara omba na kujiandaa ukiongezea mistari mingine ya Biblia
na mifano yako mwenyewe ili kufanya somo lieleweke vizuri zaidi.

 

1.  Mimi Ni Bwana Nikuponyaye

Katika Mt 9:35 tunaambiwa kwamba Yesu alipita huko na huko akihubiri, akifundisha na kuponya wagonjwa. Katika Yn 14:12 Yesu anatazamia kwamba kila anayemwamini afanye kazi anazozifanya na kubwa zaidi ya hizo! Paulo aliandika katika Rum 15:19 akisema kwamba yeye aliihubiri Injili kwa ukamilifu, kwa kusema, kutenda na kwa ishara na miujiza.

Yesu anawaamuru wafuasi wake ‘kuponya wagonjwa’ na si kuwaombea tu. Waamini wengi ulimwenguni mwote wanaelezea jinsi Bwana anavyoponya kiroho na  kimwili. Anaponya hata ndoa na matatizo ya kifedha kwa sababu lengo lake ni sisi tuwe wazima katika mwili, nafsi na roho.

2. Uponyaji Ni Katika Biblia Yote

Kama ungetumia pini na kutoboa karibu kila ukurasa wa Biblia neno lingechuruzika upendo wa Mungu na uponyaji wake.

Maradhi ni moja tu ya matokeo ya anguko, lakini tangu mwanzo Mungu anaahidi wokovu na neema (Mwa 3:15,21).

Katika Kut 3:7 tunaambiwa kwamba Mungu huona machozi yote na mateso. Yuko tayari kufanya jambo kupitia kwa mtu aliye mtiifu na tayari kutumika.

Katika Kut 15:22-26 Bwana anajidhihirisha kwa mara ya kwanza kama Bwana aponyaye. Anamwonesha Musa kipande cha mti kama picha ya Msalaba. Yatupasa kutupa kipande hicho cha mti katika maji machungu ya maisha yetu ili yabadilike kuwa matamu.

Katika Hes 21:4-9 watu wanang’atwa na nyoka kwa kosa lao wenyewe. Hata hivyo Bwana anawataka waache kuangalia majeraha yao na badala yake watazame juu ili wapate kuishi. Hii ni picha ya Ebr 12:2 ambapo tunatakiwa kuacha kuangalia ugonjwa na badala yake tumwangalie Yesu. Hatuwezi kuangalia sehemu mbili kwa wakati mmoja kama kinyonga. Yatupasa kuchagua; ama tuangalie magonjwa yetu au tuangalie ahadi ya Mungu.

Ayubu alivumilia mateso makali yasiyoelezeka mpaka hatimaye akaponywa na kupokea baraka mara mbili (Ayubu 42).

Daudi anatutahadharisha tusijesahau kuwa moja ya fadhila za Bwana ni kutuponya na magonjwa yetu yote (Zab 103:1-5).

Malaki anasema kwamba Bwana ana uponyaji katika mbawa zake (Mal 4:2).

Yesu Alikuja Kuyafanya Mapenzi Ya Baba Yake (Ebr 10:9)
Kuna mifano 26 tofauti inayomwonesha Yesu akiponya watu wenye uhitaji; na hii inatuonesha mapenzi ya Baba. Angalia somo la 8 Ishara na Miujiza.

Shuhuda tatu za kuaminika sana kwenye Biblia zinathibitisha kwamba Yesu anaponya wagonjwa.

  1. Nabii Isaya anaeleza habari za Yesu karne nyingi kabla ya kuja kwake. (Soma Isa 53:4-6).
  2. Mathayo, aliyemshuhudia Yesu kwa macho yake anasema unabii wa Isaya unatimia katika Yesu. (Soma Mt 8:17).
  3. Petro, shahidi aliyemwona Yesu, anasema unabii umetimia ndani ya Yesu. (Soma 1 Pet 2:24).

3. Uponyaji Wangu U Wapi?

"Injili yetu ni rahisi, yenye nguvu, inamhusu Kristo na imekamilika milele”.

Je, waweza kuona kwamba neno la Mungu linatuambia kuwa uponyaji wetu ulitimilizwa na Yesu pale msalabani miaka 2000 iliyopita? Pale ndipo tunapotazama kuupata uponyaji wetu; hatuangalii nyakati zijazo. Tunamwona Yesu, tunamwamini na kupokea; tunatoa shukrani kwa imani, na kupumzika, na huku tukiwiwa na Bwana kutenda kazi.

4. Je, Ni Karama Moja Kwa Mmoja Au Nyingi Kwa Wote?

Katika 1 Kor 12:9 tunajifunza kwamba Roho hutoa karama za uponyaji kwa wagonjwa. ‘Karama za uponyaji’  ni maneno yanayoonesha wingi. Hii si karama ya uponyaji ya kutumiwa na mtu mmoja, ingawaje baadhi ya wanaume na wanawake wana imani zaidi na upako zaidi kwa ajili ya huduma ya uponyaji.

Sisi Sote Twaweza Kuwaombea Wagonjwa
Unaweza ukadhani kwamba imani yako ni ndogo sana; lakini fahamu kwamba kila mmoja wetu anaweza kuombea wagonjwa kwa neema ya Mungu tuliyonayo katika wito wetu na ofisi zetu, bila kutegemea viwango vyetu vya imani.

5. Ni Nani Awezaye Kuombea Wagonjwa?

6. Jinsi Ya Kufanya Huduma Ya Uponyaji

Kwa kuongozwa na Mungu, unaweza kuwahudumia wagonjwa; mahali po pote na wakati wo wote; si lazima kusubiri mpaka wakati wa ibada au katika mikutano ya injili.

  1. Kusudia kwa kweli kuchukia magonjwa.
  2. Kusudia kwa kweli kuwapenda watu kwa kuwa tayari kuwaombea ili waponywe.
  3. Kila inapowezekana wafundishe watu kuwa na imani, ili wapate kuombeana wenyewe kwa wenyewe, vinginevyo waazime imani yako.
  4. Kila wakati mtii Roho Mtakatifu (Mdo 3:6).
  5. Msihi Mungu akufundishe jinsi ya kuomba, kwa mfano, ‘Huu ni ugonjwa, au ni pepo mchafu anayemtesa huyu mtu?’
  6. Kila mara uzifunge kwa Jina la Yesu, nguvu zote za kishetani zinazosababisha na hata kuongezea udhaifu.
  7. Usiogope kuomba dhidi ya mzizi wa ugonjwa fulani na kuuamuru uondoke kwa Jina la Yesu, kwa sababu Yeye mwenyewe ameweka shoka penye mzizi.
  8. Achilia nguvu za Mungu kwa maombi, na kwa kuwekea mikono, na hata kwa kupaka mafuta (Mk 6:13).
  9. Uvumilie na kung’ang’ania hadi ushindi umepatikana. Hata Yesu mwenyewe alimwombea mgonjwa mmoja zaidi ya mara moja.


Kwa Kumalizia Omba Kwa Ajili Ya Watu Wa Ulimwengu
Huu Ambao Bado Hawajafikiwa Na Injili; Wataje Kwa Majina
 
 

Bosnia-Hercegovina

Jina la Watu

Lugha Yao

Idadi     Yao

Rumelian Turk

Turkish

50,000

 







 1985 - 2007

With many thanks to Pastor Dastan Mboera, Dar es Salaaam, Tanzania
and EAPTC Nairobi, Kenya for this revision and translation from the original English.
mboeradsk @ yahoo.com


© Dr Les Norman  The DCI Trust, UK
Permission is granted to provide copies at cost price for study purposes
but not for sale or commercial purposes. Freely you have received, so please freely give.

Support Pages   Index To All Lessons   School of Finances  

World Christian News   
Who Are We?   Site Index

www.dci.org.uk